Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MALINZI KUMLIPA POULSEN ILI AONDOKE

Rais  wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, amesema atalipa nusu ya gharama zilizotokana na shirikisho hilo kuvunja mkataba wa aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen.

Hata hivyo, Malinzi na Kim hawakutaka kuweka wazi hatua walizofikia baada ya kuamua kuvunja mkataba zaidi ya kueleza kuwa walifikia makubaliano ya pamoja.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Malinzi alisema sehemu nyingine ya gharama ya fedha zilizobakia zitalipwa na shirikisho hilo na waliamua kusitisha mkataba wa Kim ili wasake kocha mpya ambaye moja ya sifa zake ni kuwahi kuipeleka timu mojawapo ya Afrika kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON.


Malinzi alisema serikali haihusiki na maamuzi hayo yaliyofikiwa na TFF ila ilijulishwa hatua zote za mchakato huo na kuelezwa tayari wameshaanza kusaka kocha atakayerithi mikoba ya Mdenmark huyo.

"Tulichokubaliana ni siri na kitabaki kuwa siri, TFF tutabeba, wapo wadau waliojitokeza kutulipia nusu kwa sababu waliahidi kuwa huu ni wakati wa mabadiliko," alisema Malinzi na baadaye kubadili kauli ya wadau na kujitaja yeye kuwa ndiye atakayelipa gharama hizo.

Aliongeza kwamba tayari TFF imeshabaki na majina matatu (hakuyataja) ya makocha ambao mmoja wao ataajiriwa akisema wawili wanatoka Uholanzi na mwingine ni raia wa Ujerumani.

"Jukumu lake kubwa litakuwa ni kuendeleza soka la vijana na atachagua msaidizi wake," aliongeza.

Alimtaja Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi, ambaye ana leseni Daraja A kuwa ndiye atakaimu nafasi ya Poulsen na ataiongoza Taifa Stars katika mechi moja itakayochezwa Machi 5 jijini Windhoek, Namibia.

POULSEN ANENA

Naye, Poulsen  aliwashukuru wachezaji, benchi la ufundi, wadhamini (Kampuni ya Bia Tanzania- TBL), mashabiki na wadau wote wa soka nchini kwa kumpa ushirikiano katika kipindi chote alichokuwa hapa nchini tangu Mei, 2012.

"Kunapokuja uongozi mpya lazima vitu kama hivi hutokea, uongozi mpya wa TFF umefanya mabadiliko mengi katika uongozi wake, hivyo hata mimi sishangai kuona nafukuzwa ingawa nimesaidia kwa kiasi kikubwa kuleta mafanikio ya soka la Tanzania," alisema Poulsen.

Raia huyo wa Denmark alisema alikuta Tanzania ikiwa nafasi za chini katika viwango vya Fifa lakini sasa iko nafasi iko vizuri na ameiwezesha Taifa Stars kuzifunga timu ngumu za Zambia, Cameroon na Morocco.

"Kuna baadhi ya mechi tulifungwa kwa sababu ya mazingira yetu, mnakwenda kucheza  na timu ngumu huku wachezaji wenu hawana lishe ya uhakika, tuliangushwa na lishe katika mechi ya mwisho ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia," alisema Poulsen.

Alisema hata hivyo anaheshimu maamuzi ya viongozi wapya wa TFF ambao wanaamini wako sahihi.

Poulsen aliishukuru ajira aliyokuwa nayo Stars kwamba imemwezesha kupata kazi ya ukufunzi wa makocha wa FIFA na akaongeza atakuwapo nchini hadi atakapolipwa fedha zake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Alfred Kidau, alisema idara yake iko wazi na mabadiliko yaliyofanywa kwenye benchi la ufundi yalikuwa ni ya nia njema.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC