Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA WA YANGA AAPA KUIUMALIZA MAPEMA AL AHLY

Na Regina Mkonde, Bagamoyo

Kocha mkuu wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, Yanga, Mholanzi Hans van der Pluijm, amesema atahakikisha anatumia mbinu zote alizo nazo ili kuiondoa Al Ahly ya Misri kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kuifanya ajira yake iendelee kuwapo ndani ya Wanajangwani hao.

Akizungumza juzi jioni baada ya timu hiyo kufika Bagamoyo mkoani Pwani, Pluijm alisema aliufahamu 'mtihani' huo wa kukabiliana na Al Ahly mapema kabla ya kuja nchini kukubali ajira ya kuifundisha Yanga.

Pluijm alisema katika soka hakuna kitakachoshindikana na akaongeza dakika 180 ndizo zitakazoamua nani atasonga mbele.

Mholanzi huyo alisema katika dunia ya sasa kwenye soka hakuna mechi rahisi au mashindano mepesi na kwamba kila upande unajiandaa kufanya vizuri na kuweka rekodi.


"Najua sasa macho yote Yanga na wadau wengi wa soka wa Tanzania wanasubiri siku ifike, nilifahamu na nilianza mapema maandalizi ya kuwakabili hao mabingwa wa zamani wa Afrika, ila na mechi za ligi ya ndani ni muhimu na tutataka kushinda, " alisema kocha huyo.

Alieleza kwamba endapo wachezaji wake watakuwa 'fiti' ana hakika wataonyesha kiwango bora na hakuna atakayepata ushindi bila ya kupambana.

Aliongeza kuwa, kushinda katika mechi ya kesho ya ligi dhidi ya Ruvu Shooting kutawaongezea morali wachezaji wake ambao nao wanaiwaza Al Ahly.

Kama walivyofanya Al Ahly kuleta 'mashushu' wake kuipeleleza Yanga ilipokuwa inacheza na Komorozine ya Comoro katika mechi yake ya kwanza ya mashindano hayo ya kimataifa, wawakilishi hao pekee wa Tanzania waliobakia kwenye michuano ya Afrika, kocha msaidizi  Boniface Mkwasa, naye yuko jijini Cairo akiwasoma wapinzani wao.

Yanga ilisonga mbele katika mashindano hayo ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka huu baada ya kuitoa Komorozine kwenye hatua ya awali kwa jumla ya mabao 12-2.

Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngasa, ndiye anayeongoza kwa kupachika mabao katika mashindano hayo yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) baada ya kufunga hatrick mbili nyumbani na ugenini dhidi ya Wacomoro hao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC