Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHELSEA YAKABWA KOO NA WEST BROM 1-1

Wachezaji wa West Brom
Chelsea imepoteza nafasi ya kuhakikisha kuwa imesalia kileleni mwa ligi kuu ya Premier ya Uingereza, mbele ya mahasimu wao Arsenal, baada ya kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na West Brom, katika mechi iliyochezewa katika uwanja wa Hawthorns.

Victor Anichebe aliifungia West Brom bao hilo muhimu kunako dakika ya 87 Na kuinyima Chelsea alama mbili ambazo zingeihakikishia Chelsea hakikisho la uongozi wa ligi hiyo hadi juma lijalo.

Branislav Ivanovic aliiweka Chelsea mbele dakika ya 45, bao ambalo lilikuwa limeipa vijana hao wa Jose Mourinho kuwa alama nne mbele ya Arsenal ambayo kwa sasa inashikilia nafasi ya pili.


Arsenal imeratibiwa kucheza na Manchester United, siku ya Jumatano usiku na ikiwa Arsenal itashinda mechi hiyo itajihakikisha nafasi ya kwanza kwenye msururu wa ligi hiyo inayokwenda mapunzikoni mwishoni mwa juma hili ili kuruhusu mechi za kuwania kombe la FA.
Wachezaji wa Arsenal

Matokeo zaidi

Katika matokeo mengine ya mechi za ligi kuu zilizochezwa hiyo jana, Southampton iliilaza Hull City bao moja kwa bila.

Mlinda lango wa Southampton, Jose Fonte ndiye aliye bahatika kufunga bao hilo kufuatia purukushani katika lango la Hull City.\

Dakika chache baada ya kufunga bao hilo, Fonte alivurumisha kombora kali ambalo liliokolewa na kipa wa Hull Jay Rodriguez.
Kocha Sam Allardyce
West Ham imepanda hadi nafasi ya kumi kwenye jadwali ya ligi hiyo baada ya kuilaza Norwich kwa magoli mawili kwa bila.

Ushindi huo ulikuwa wa tatu mfululizo kwa timu hiyo iliyo na makao yake Mashariki mwa jiji la London.
Norwich kwa upande wake inashikilia nafasi ya kumi na sita alama moja mbele ya West Brom na Sunderland iiliyo katika nafasi ya kumi na saba na kumi na nane mtawalia.

Cardif nayo imesalia katika nafasi ya mkia baada ya kutoka sare ya kutofungana bao lolote na Aston Villa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC