Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM YAHAMISHIA HASIRA ZAKE LIGI KUU BARA.

AZAM FC sasa inaelekeza nguvu zake katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya jana kutolewa mapema katika michuano ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika.

Timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake, yenye maskani yake Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam, jana ilifungwa mabao 2-0 na wenyeji Ferroviario Beira kwenye Uwanja wa Ferroviario Beira mjini Beira Msumbiji katika mchezo wa marudiano, Raundi ya Awali, Kombe la Shirikisho.

Katibu Mkuu wa Azam FC, Nassor Idrisa ‘Father’ amesema kwamba matokeo hayo yamewaumiza, lakini wanalazimika kukubaliana nayo kwa sababu huo siyo mwisho wa maisha.


“Ni huzuni tu hapa, kuanzia kwa viongozi, wachezaji, benchi la Ufundi na wote katika msafara wetu. Lakini tunafarijiana hivyo hivyo, huu si mwisho wa maisha, kama kuna sehemu tulikosea, basi tumepata somo na tutajirekebisha,”alisema Father.

Alisema kwamba timu inarejea leo Dar es Salaam kuendelea na mazoezi kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu, dhamira ikiwa ni kutwaa ubingwa na kufuta machungu ya matokeo ya michuano ya Afrika.

Imetuuma, lakini ndiyo soka; Katibu wa Azam FC, Nassor Idrisa 'Father' kushoto akiwa na kiongozi mwingine wa Azam FC, Abubakar Mapwisa kushoto
“Tulitengeneza nafasi nyingi za kufunga Dar es Salaam, lakini tukafunga bao moja tu, hilo ndilo lililotugharimu, ila  si vibaya ndiyo soka, sisi wa Azam ni kitu kimoja, tunashikamana na wachezaji wetu na kwa pamoja na tunaelekeza nguvu zetu kwenye Ligi Kuu,”alisema.

Aidha, Father aliwaomba radhi mashabiki na wapenzi wa Azam FC na kuwataka wawe wavumilivu, kwa kuwa dhamira ipo ya kufanya vyema kwenye michuano ya Afrika, basi iko siku nafsi zao zitafarijika.

Katika mchezo wa jana, uliofanyika sambamba na mvua kali iliyoharibu mandhari ya Uwanja, wenyeji walipata bao moja kila kipindi, yote yakifungwa na mshambuliaji wake hatari, Mario Simamunda dakika ya tano na ya 70.

Matokeo hayo yanaifanya Azam itolewe kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya awali kushinda bao 1-0 mjini Dar es Salaam, bao pekee la mshambuliaji Kipre Herman Tchetche Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
  
Aidha, matokeo hayo pia yanamaanisha, Azam imeshindwa kufikia rekodi yake ya mwaka jana katika michuano hiyo, ilipotinga hatua ya 16 Bora na kutolewa na AS FAR Rabat ya Morocco chini ya kocha Muingereza, Stewart John Hall, aliyejiuzulu Septemba mwaka jana.

Matokeo hayo pia, yanamaanisha kocha Mcameroon Joseph Marius Omog ameshindwa kuendeleza rekodi yake nzuri aliyotoka nayo Kongo Brazaville, akiiwezesha Leopard FC kutwaa Kombe la Shirikisho.

Azam FC inaongoza Ligi Kuu ya Bara kwa pointi zake 36, ikifuatiwa na mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 35 sawa na Mbeya City iliyo nafasi ya tatu, wakati Simba SC yenye pointi 32, ipo nafasi ya nne.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC