Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ASKARI WA JKT WAUA SIMBA TAIFA, LAMBALAMBA YALAMBWA NA ASKARI MAGEREZA.

SIMBA SC imelambwa mabao 3-2 na JKT Ruvu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Azam FC imelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Prisons ya Mbeya Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Matokeo hayo yanamaanisha, Yanga SC iliyoshinda 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting jana Uwanja wa Taifa, inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 38, Azam ya pili 37 na Mbeya City ya tatu 35 na Simba SC ya nne 32.

Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam hadi mapumziko JKT Ruvu walikuwa mbele kwa mabao 2-0 yaliyotiwa kimiani na Hussein Bunu dakika ya 14 na Emmanuel Swita dakika ya 44 kwa penalti, baada ya Henry Joseph kumuangusha Amos Mgisa kwenye eneo la hatari.


Hata hivyo, penalti hiyo ilionekana kuwa ya utata, kwani mguu wa Henry ulionekana kwenda kuuondosha mpira miguuni mwa Mgisa bila kumgusa mchezaji huyo.

Kipindi cha pili, JKT Ruvu ilionekana kurudi na moto wake tena na kufanikiwa kupata bao la tatu mapema dakika ya 52, mfungaji Emmanuel Swita tena kwa shuti kali baada ya pasi ya Amosi Mgisa.

Simba SC ilizinduka baada ya  bao hilo na kupambana hadi kupata mabao mawili yaliyofungwa na Mrundi Amisi Tambwe dakika za 64 kwa penalti baada ya Amri Kiemba kuangushwa kwenye eneo la hatari na dakika ya 84, akiunganisha krosi ya Kiemba.

Uwanja wa Azam Complex, hadi mapumziko hakukuwa na timu iliyopata bao, lakini kipindi cha pili, Prisons walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Omega Seme anayecheza kwa mkopo kutoka Yanga SC dakika ya 47 kwa shuti la mpira wa adhabu baada ya Aggrey Morris kumchezea rafu Jimmy Shoji.

Aggrey Morris akaisawazishia Azam FC dakika ya 50 kwa kichwa baada ya kuuwahi mpira uliorudishwa na beki wa Prisons kufuatia John Bocco kuunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu wa Erasto Nyoni.

Azam FC walionekana kuwa katika nafasi ya kuondoka na pointi tatu baada ya Kipre Herman Tchetche kuifungia bao la pili timu hiyo dakika ya 51 kwa shuti kali baada ya kuiwahi pasi ndefu ya Nyoni.

Kipre Tchetche alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 58 baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na refa Alex Mahagi wa Mwanza kwa kuushika mpira makusudi ili kuuweka sawa.

Hata hivyo, zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo huo kumalizika, Laurian Mpalile aliisawazishia Prisons dakika ya 88 baada ya pasi nzuri ya Freddy Chudu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC