Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WENGER AICHEKELEA CARDIFF ISIYO NA KOCHA.

Arsenal wana nafasi ya kuimarisha uongozi wao wa Ligi ya Premier ya Uingereza ikiwa watawachakaza Cardiff City, ambao hawana meneja, kwa mara ya pili katika kipindi kichache wakati shindano hilo litakapo rejea siku ya kuadhimisha Mwaka Mpya.

Ligi ya Premier iko katika pilika pilika za mechi ya nne ndani ya siku kumi wakati ambao wachezaji na vilabu vya nchi zingine barani Uropa viko kwenye mapumziko ya sherehe za Krismasi.

Huku ligi hiyo ikiwa imefikia kati musimu huu baada ya raundi 19 kusakatwa, Arsenal wanamiliki uongozi na alama 42, ikiwa ni mara ya kwanza kilabu hicho kuanza mwaka kileleni tangu kampeni ya 2007-08.


Manchester City (41), Chelsea (40) na Everton (37) wanawaandama katika nafasi nne bora.

Kinyang’anyiro cha mwaka huu kimechacha moto kwani Liverpool walioongoza Krismasi wameshuka ngazi hadi nafasi ya 5 na pointi 36 baada ya kupoteza dhidi ya City na Chelsea.

Vijana hao wa Brendan Rodgers ambao wataalika Hull City wamo alama mbili mbele ya mabingwa Manchester United na Tottenham Hotspur ambao watagaragazana uga wa Old Trafford Jumatano.

Katika nafasi za mwisho, pointi saba pekee zimetofautisha Swansea (21) katika nafasi ya 11 na Sunderland wanaovuta mkia.

Kwenye barua yake kwa mashabiki ya kila wiki, meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amenena kwamba kuna “kitu specheli” na kikosi chake cha sasa huku akisifu weledi wao wa kimawazo, “hili jambo limezua maswali mara mengi hapo awali.”

“Tulithihirisha hilo ugenini West Ham pale tulijiinua kutoka kufungwa 1-0 na kushinda 3-1 na turirudia tena Newcastle pale tulipofanikiwa kushinda 1-0 ingawa tulijipata hayawani katika dakika 15 za mwisho.”

“Kuna umoja na roho juu sana kikosini.”

Wenger anazungumuza na uzoefu kwani Arsenal ni miongoni mwa timu tatu zilizoongoza Mwaka Mpya lakini wakakosa kutia taji kibindoni katika mwongo mmoja uliopita.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...