Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UGANDA YATISHWA NA MAKALI YA SAMATTA, ULIMWENGU, POULSEN ATAMBA USHINDI LEO.

ROBO Fainali za kwanza za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Chalenge zinatarajiwa kuchezwa leo Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya.

Mechi inayotarajiwa kuteka hisia za wengi ni kati ya mabingwa watetezi, Uganda The Cranes dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars itakayoanza saa 8:00 mchana, ingawa kutakuwa na mchezo mwingine kati ya Kenya na Rwanda saa 10:00 jioni.

Stars wanaingia katika sura ya unyonge kumenyana na The Cranes inayofundishwa na kocha hodari Afrika, Mserbia Milutin Sredojevic ‘Micho’ kutokana na kufungwa mfululizo na wapinzani wao hao siku za karibuni.

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayoundwa na idadi kubwa ya wachezaji wa Bara ilifungwa nyumbani na ugenini na Uganda katika mechi za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za CHAN.


Lakini pia, Uganda imeonyesha ni tishio katika Challenge ya mwaka huu baada ya kufuzu Robo Fainali kwa kushinda mechi zake zote za Kundi C, wakati Bara ilipata ushindi mwembamba wa 1-0 mara mbili na sare moja hivyo kushika nafasi ya pili Kundi B.

Kocha Mdenmark, Kim Poulsen amesema kwamba anawaheshimu Uganda ni timu nzuri na anatarajia mchezo utakuwa mgumu, lakini yeye amewaandaa vyema vijana wake kushinda mechi ya leo.

Micho pia amesema Stars ni wazuri hasa baada ya kuwasili kwa washambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao amesema wakiungana na Mrisho Ngassa watetengeneza safu kali ya ushambuliaji.

Kwa ujumla makocha wote wanaogopana kuelekea mchezo huo- jambo ambalo linaashiria hiyo ni mechi isiyotabirika hata chembe.

Kama alivyosema Micho, safu ya ushambuliaji ya Stars leo inatarajiwa kuongozwa na Ngassa, Ulimwengu na Samatta wakati viungo wanaweza kuwa Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na Athumani Iddi ‘Chuji’.
Langoni ataanza Ivo Mapunda, kulia Himid Mao, kushoto Erasto Nyoni na katikati Said Morad na Kelvin Yondan.

Kwa upande wa mabingwa watetezi, Uganda, Emanuel Okwi, Hamisi Kiiza na Dani Sserunkuma wanatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji, wakati wengine kikosini watakuwa Nico Wadada, Godfrey Kizito, Khalid Aucho, Brian Majwega, Vincent Kayizzi, Godfrey Walusimbi, Savio Kabugo na Benjamin Ochan langoni.
      
Emmanuel Okwi ndiye tegemeo la mabao la Uganda Challenge
Kenya inapewa nafasi kubwa ya kuitoa Rwanda katika mchezo wa pili. Je, Stars itafuta uteja kwa The Cranes leo?

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC