Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIRI YAGUNDULIKA KINACHOMUONDOA MANJI YANGA.

Na Salum Fikiri Jr

HATIMAYE siri imegundulika kwamba kinachomuondoa mwenyekiti wa mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga Yusuf Manji kufuatia kauli yake aliyoitoa jana wakati viongozi wa timu hiyo walipokutana na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuteua wajumbe wengine katika kamati mbalimbali zilizoundwa.

Siri iliyogundulika na kuelezwa Mambo Uwanjani kuwa mwenyekiti huyo atogombea tena Uenyekiti katika uchaguzi ujao na kuwapisha wengine wenye nia ya kutaka kuiongoza Yanga, lakini inasemekana Manji amekimbia kivuli chake huku suala la mheshimiwa Rage na klabu yake ya Simba moja kati ya sababu zinazomuondoa mapema Yanga.

Mbali na hilo msimamo wa baraza la wazee la klabu hiyo linaloongozwa na mzee Ibrahim Akilimali ambalo lilipinga waziwazi ajira ya Mkenya kuwa katibu mkuu wa Yanga pamoja na mtunza fedha ambaye alikuwa Mhindi, wazee hao waliendelea na msimamo wao na kupinga wazo la kuanzishwa kwa kampuni.


Inadaiwa wazee hawakutaka Yanga igeuzwe kampuni kitendo ambacho kilitaka kufufua mgogoro mkubwa kama ule wa mwanzo ambao ulizaa Yanga kampuni na Yanga asili, Hivyo Manji akaona Yanga haitawaliki na ni bora atangaze kujiondoa mapema na kuwapisha wengine kuongoza.

Chanzo chetu cha habari ambacho kipo karibu na watu wa timu hiyo kimesema kuwa maamuzi ya Manji yanatokana na sababu hizo, 'Manji alitaka Yanga iwe kampuni ili yeye aweze kununua hisa nyingi na kuimiliki timu hiyo kama ilivyo kwa timu nyingine kubwa za huko Uingereza ambazo zinaendeshwa na mfanyabishara mmoja tajiri.

Man United inaye Glazzer, wakati Chelsea inaye Abramovich, na Yanga ilitakiwa iwe na Manji, kilisema chanzo hicho, Aidha mwenyekiti huyo wa Yanga amekasirishwa na mambo mengi yanayofanyika klabuni hapo ikiwemo wazee kujifanya wao ndio wasemaji wa klabu badala ya mwenyekiti ambaye ni yeye na afisa habari wao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC