Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MKOLA MAN AHUSISHWA NA FREEMASON, NEMBO YAMPONZA.

Na Exipedito Mataluma


MWANAMUZIKI wa kizazi kipya anayetokea Hale mkoani Tanga Christopher Mhenga maarufu Mkola Man anatajwa kuwemo katika orodha ya wasanii wanaotajwa kuwemo kwenye imani ya kishetani inayoenea kwa kasi nchini ya 'Freemason' huku ikidaiwa nembo anayotumia ndio imemponza.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari vinasema kuwa msanii huyo kwa sasa ameanza kujipatia umaarufu mkubwa na kupata mialiko kadhaa ndani na nje ya Tanzania kiasi kwamba kinawachanganya wengi, pia kuongezeka kwa mashabiki na kupendwa kwa nyimbo zake ukiwemo huu mpya wa 'Kilevi changu' ni sehemu nyingine inayotajwa kuwemo katika imani hiyo.

Pia chanzp chetu kimefichua siri ya msanii huyo kuwa anatumia nembo maarufu ya '5LAMABAD' ambayo ni moja kati ya alama za imani hiyo, kitu kingine kilichoibua tetesi za msanii huyo kujihusisha na freemason ni pale alipopiga picha akifanya tambiko kwenye makaburi ambapo inasemekana watu wenye imani hiyo hupendelea kufanya hivyo.


Baadhi ya wakazi wa Tanga ambao wanamfahamu msanii huyo anayetajwa kutikisa jiji hilo kwa sasa na kuwapiga kumbo wakongwe kadhaa waliokuwa wakitamba katika jiji hilo kama Seif Shaaban Matonya na Wagosi wa Kaya wanadai kuwa Mkola Man anaponzwa na jina lake.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mkazi mmoja wa Tanga (Jina kapuni) amedai katika kitabu tukufu cha Biblia jina la Mkolar Man ni la kishetani na linatumiwa zaidi na watu waharifu kama vile majambazi, wauaji, wacheza kamali na ngono.

Pia jina hilo kwa lugha ya kiswahili ni sawa na mtu mkorofi, gaidi na mhuni wa kutupwa, aidha mwandishi wetu alipata taarifa nyingine ya siri kuwa msanii huyo ni mwanachama wa genge hilo na tayari amewasaidia wasanii mbalimbali hapa nchini kujiingiza katika imani hiyo potofu na inayokemewa na viongozi wa dini mbalimbali nchini.

Aidha Mambo Uwanjani ilimtafuta kwa niia ya simu msanii huyo ili aweze kutoa uthibitisho wake bahati mbaya simu yake ilikuwa haipatikani huku jitihada za kumpata zikiendelea.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...