Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MESSI HATOENDA KOKOTE-ROSELL.

Staa matata wa Barcelona, Lionel Messi, hataenda popote katika utawala wa rais Sandro Rosell kiongozi huyo alitangaza Alhamisi.

"Kwa muda wote nitakuwa rais, lolote liwezekanalo au lisilowezekana litatendwa kuhakikisha Messi anasalia kitako hapa," Rosell alihimiza katika hafla ya kuwasilisha mkataba wa ushirikiano baina ya Barca na kampuni kuu ya elektroniki ya Marekani, Intel.

"Ni vigumu sana, au tuseme haitowezekana, kuwa Messi ataondoka timu hapa."

Mshindi mara nne wa tuzo la Ballon d' Or anauguza jeraha na anatarajiwa kurudi uwanjani Januari huku kandarasi yake Barcelona ikidumu hadi 2018 karibu na wakati nyota huyo atakuwa karibu kuadhimisha miaka 31 tangu kuzaliwa kwake.


Tetesi kuhusu hatima yake zilizuka Jumanne pale makamu wa rais wa maswala ya kiuchumi Barca, Javier Faus, alipofichua hakuna haja ya kujadilia kandarasi yake upya.

"Kwanini? Kandarasi yake Ilijadiliwa upya miezi sita pekee iliyopita," Faus aliambia kituo cha redio cha Rac1.

Kulingana na duru Uhispania, Messi ana kipengee cha Euro milioni 250 kwa yeyote anayetamani kumtia huru kutoka minyororo ya kandarasi yake na Barca injawaje timu zenye uwezo wa kutimiza hayo ni chache muno.

Uvumi kuhusu uwezekano wa mazungumzo mapya baina ya mshambuliaji huyu na klabu chake umezuka kutokana na swala la mishahara.

Mtana shari wake Real Madrid, Christiano Ronaldo, alisaini mkataba mpya wenye dhamani ya Euro milioni 17 kila mwaka kulingana na gazetu la Marca kumfanya awe mchezaji kabumbu anayelipwa kiasi kikubwa nchini hiyo.

Jarida la Forbes linashikilia Messi anatia kibindoni Euro milioni 16 kila mwaka kwa ulinganishi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC