Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUNANI YANGA! NGASA, MSUVA WATIMKA.

Yanga imepata pigo baada ya winga wake, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na beki wa kati Nadir Haroub 'Cannavaro' kuugua jambo litakalowafanya kuwa nje ya uwanja kwa siku kadhaa, hivyo kuzikosa mechi za mwanzo za michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoanza kesho visiwani Zanzibar.

Katika ratiba iliyotolewa na waandaaji wa michuano hiyo, inaonyesha Yanga itaanza kwa kucheza dhidi ya Tusker ya Kenya keshokutwa.
Ngasa anasumbuliwa na homa ya matumbo wakati Cannavaro ni majeruhi wa goti huku Simon Msuva akisumbuliwa na malaria.

Hali hiyo ilimfanya Ngasa kuyakosa mazoezi ya Yanga yaliyofanyika kwa saa mbili jana kuanzia saa 3:00 - 5:00 asubuhi chini ya Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Felix Minziro. Wachezaji wengine ambao hawakuwapo jana ni pamoja na washambuliaji Waganda, Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza, winga Msuva na kiungo Salum Tetela.


Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Daktari wa Yanga, Nassoro Matuzya, alisema Ngasa anasumbuliwa na maradhi ya tumbo na atakuwa nje ya uwanja kwa takriban wiki nzima ili kukamilisha dozi ya dawa aliyoianza juzi.

"Ngasa alipimwa jana (juzi) na kugundulika kusumbuliwa na maradhi ya tumbo. Ameanza kumeza dawa ambazo dozi yake itakamilika ndani ya siku tano. Baada ya hapo tutaangalia kama kutakuwa na uwezekano kuungana na wachezaji wenzake katika timu," alisema Matuzya.

"Msuva naye hajisikii vizuri leo (jana) na mchana huu atafanyiwa vipimo vya afya kwenye Hospitali ya Mwananyamala. Telela na Cannavaro (Nadir Haroub) nao hawako vizuri na wako nje ya kikosi. Telela ni majeruhi kwa muda mrefu na atarejea uwanjani Ijumaa. Cannavaro anasumbuliwa na jeraha la goti," alifafanua zaidi daktari huyo.

Yanga, ambao wanasaka kocha mpya baada ya kutangaza kuachana na Mholanzi Ernie Brandts aliyewapa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu uliopita, wamepangwa Kundi C katika Kombe la Mapinduzi, michuano itakayoshirikisha timu 12, pamoja na mabingwa watetezi, Azam FC, Tusker ya Kenya na Unguja Combine.

Kundi A kuna Mbeya City, Pemba Combine, Chuoni na URA kutoka Uganda wakati Kundi B lina timu za Simba, KMKM, AFC Leopards ya Kenya na KCC ya Uganda.

Pazia la mashindano hayo litafunguliwa kesho kwa mechi mbili za Kundi B kwenye Uwanja wa Amaan, saa 10:00 alasiri kwa mabaharia wa KMKM kupambana na Manispaa ya jiji la Kampala (KCC).

Aidha, saa 2:00 usiku, 'Wekundu wa Msimbazi', Simba, watakuwa kibaruani dhidi ya AFC Leopards.

Keshokutwa kutakuwa na mechi nne kwenye viwanja vyote viwili vya Amaan, Unguja na Gombani, Pemba. Uwanja wa Amaan kutakuwa na mchezo kati ya mabingwa watetezi Azam FC dhidi ya Unguja Combine kuanzia saa 10:00 alasiri na Yanga dhidi ya Tusker itakayorindima kuanzia saa 2:00 usiku.

Uwanja wa Gombani shughuli itakuwa kati ya URA na Chuoni (Kundi C) watakaovaana saa 8:00 mchana huku Mbeya City ikitoana jasho na Pemba Combine kuanzia saa 10:00 jioni katika mchezo wa Kundi A.

Fainali ya michuano hiyo itapigwa Uwanja wa Amaan Januari 12 kuanzia saa 2:00 usiku, siku ambayo ndiyo kilele cha maadhimisho ya sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wakati huo huo, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh, alisema hadi jana mchana walikuwa hawajafahamu wataondoka lini kuelekea Zanzibar licha ya kufahamu mechi yao ya kwanza itachezwa keshokutwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC