Ruka hadi kwenye maudhui makuu

IVO MAPUNDA ASAINI SIMBA MIAKA MIWILI.


Uongozi wa Simba umesema upo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kipa mkali wa kupangua mikwaju ya penalti Mtanzania Ivo Mapunda.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope alisema uongozi wa 'Wanamsimbazi' hao

umekubaliana kumpa mkataba wa miaka miwili kipa huyo wa zamani wa watani wao wa jadi, Yanga.

"Kwa sasa tunamsikiliza kocha (Mcroatia Zdravok Logarusic) kama kuna mchezaji mwingine anayemhitaji baada ya kumpata Ivo.

Tumekubaliana tumpe mkatana wa miaka miwili ambao atausaini mara tu baada ya mashindano ya Kombe la Chalenji," alisema Hanspope.

Alisema wametenga fungu nono ambalo limemshawishi nyota huyo kujiunga nao.


Hata hivyo, Hanspope hakuwa tayari kuweka wazi kiasi cha fedha za usajili na mshahara ambao Ivo atakuwa akilamba katika klabu hiyo ambayo kwa sasa inakabiliwa na mgogoro wa uongozi.

Simba imeonekana kutoridhishwa na kiwango cha kipa wake Mganda, Abel Dhaira baada ya kuamua kumsajili kwa muda wa miezi sita kipa wa zamani wa Yanga, Mgana Yaw Berko na sasa inamalizia usajili wa kipa mzawa Ivo.

Kipa huyo aliyeipa ubingwa wa Ligi Kuu ya Kenya klabu yake ya sasa ya Gor Mahia msimu uliopita na kujizolea umaarufu wa kupangua michomo ya penalti nchini humo, Jumamosi alidaka penalti mbili kati ya tatu walizokosa Uganda na kuiwezesha Timu ya Taifa ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Kombe la Chalenji. 

Mashindano hayo yalianza Novemba 27 na yatafikia tamati Desemba 12, mwaka huu yakishirikisha timu za taifa za nchi 11 za Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati huku mabingwa wa zamani wa Afrika, Zambia wakishiriki kama timu alikwa.

Kanuni mpya ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) inayozitaka timu kuwa na wachezaji wa kigeni wasiozidi watatu na makipa wazawa kuanzia msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, huenda ikailazimu Simba kuachana na Dhaira na Berko na kubaki na Ivo na makipa wengine wazawa ili kukidhi matakwa ya Azimio la Bagamoyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC