Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DORTMUND, MILAN WACHECHEMEA HADI 16 BORA .

Borussia Dortmund ambao walimaliza wa pili msimu uliopita waliepusha aibu ya kubanduliwa mapema Ligi ya Klabu Bingwa na bao la dakika za lala salama lake Kevin Grosskreutz ambalo liliwafikisha Wajerumani hao hadi kwenye 16 bora Jumatano.

Dortmund, ambao waliilaza Olympique Marseille 2-1, Arsenal na Napoli wote walimaliza wakiwa na alama 12 huku timu hiyo ya Bundesliga ikimaliza ya kwanza Kundi F na Wataliano hao kuibuka wasio na bahati na kutemwa kutokana na mechi za moja kwa moja licha ya ushindi wa 2-0 dhidi ya viongozi hao wa Ligi ya Premia Uingereza.

AC Milan watakuwa ndio wawakilishi pekee wa Italia katika awamu ya muondoano. Galatasaray, Zenit St Petersburg na Schalke 04 walijaza nafasi zilizosalia katika 16 bora na watakuwa kwenye droo ya Jumatatu ambayo itakuwa na wawakilishi wane kutoka Ligi ya Premia na kutoka Bundesliga.

Barcelona, ambao wanatarajiwa kuwa na Lionel Messi anayeuguza jeraha dimba litakaporejelewa Februari, walimaliza awamu ya makundi kwa njia ya kipekee huku straika wa Brazil Neymar akiwafungia mabao matatu, yake ya kwanza katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, na wakacharaza Celtic 6-1 uwanjani Nou Camp.

Jose Mourinhoanaweza kusubiri kwa hamu droo kwani Chelsea walishinda Kundi E baada ya kucharaza Steaua Bucharest 1-0 uwanjani Stamford Bridge.

Napoli, ambao sasa watacheza Europa League, ndio wa pili kuwahi kubanduliwa katika awamu ya pili licha ya kuwa na alama 12 kutoka kwa mechi sita wengine wakiwa Paris St Germain waliobanduliwa 1997-98.

Katika hali tofauti kabisa, Zenit kutoka Urusi ambao walimaliza wa pili katika Kundi G ndio wa kwanza kufuzu kwa awamu ya muondoano wakiwa na alama sita.

Dortmund wanaohangaishwa na majeraha walikuwa wamebakia na dakika chache sana kabla yao kutupwa dimba la ngazi ya pili Ulaya pale Grosskreutz alipoona wavu kwa kombora ambalo lilipinduliwa dakika tatu tu kabla ya mechi kuisha wakicheza dhidi ya wachezaji 10 wa Marseille.

"Ilikuwa ni furaha sana kufunga bao kama hilo. Tulistahili, lilikuwa la kufurahisha sana,” alisema mfungaji bao huyo.

Galatasaray walifikisha kikombo safari ya mabingwa wa Italia Juve kwa ushindi wa 1-0 mjini Istanbul, Wesley Sneijder akifunga bao la ushindi dakika za mwisho kwenye mechi ambayo ilirejelewa Jumatano baada ya kusimamishwa Jumanne kutokana na theluji.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...