Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHELSEA WAMEKOSA MAKALI YA KUUA- MOURINHO

Meneja wa Chelsea Jose Mourinho alilazimika kurudia tena hadithi yake ya kawaida huku akiomboleza kushindwa kwa timu yake kufunga baada ya kubanduliwa kwa kulazwa 2-1 muda wa ziada na Sunderland katika League Cup Jumanne.

"Kiwango cha uchezaji soka ambacho tulionyesha ni kizuri sana. Hatushindwi kwenye mechi kwa sababu eti hatuchezi au kwamba mpinzani anatuzidi, ni kutokana na hali kwamba hatuui wapinzani wetu na tunawapa uhai,” Mourinho aliambia Sky Sports baada ya timu yake kubanduliwa katika robofainali.

“Kila mpinzani anajua kwamba anaweza kutufunga bao. Tulipata nafasi nyingi nzuri za kufunga na hatukufunga.”

Ingawa Chelsea wako nambari tatu kwenye Ligi ya Premia na wako awamu ya muondoano katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, matokeo ya kushangaza majuzi yamefanya Mourinho kutahadhari zaidi kuhusu uwezekano wa timu yake kushinda mataji.


Kushindwa mara mbili na kutoka sare katika mechi saba za Ligi ya Premia pamoja na kushindwa mara mbili za Basle ya Uswizi, nyumbani na ugenini Ulaya, kumewafanya wengi kuangazia mastraika butu Fernando Torres, Demba Ba na Samuel Eto'o.

Watatu hao wamefunga mabao matano pekee kwa jumla msimu wote.

Eto'o ambaye alikabidhiwa jukumu la kuongoza mashambulizi dhidi ya Sunderland alipoteza nafasi nzuri ya kufunga bao la pili kipindi cha pili baada ya kuachwa yeye na kipa pekee.

Alipoulizwa ni kwa nini timu yake ya sasa Chelsea haikosi huruma kama ile aliyokuwa nayo kipindi cha kwanza alipokuwa kwenye klabu hiyo, Mourinho alisema: "Siwezi kujibu swali hili.

Mimi ni meneja wa timu hii na si ile ya awali. Hatuko nyuma ya timu hiyo ya awali, lakini tuko mbele ukiangalia kiwango.

“Lakini soka ni kuhusu matokeo na kufunga mabao. Kulikuwa na nafasi nyingi nzuri na si moja pekee. Tulitaka sana kuendelea katika dimba hili lakini hatukulipa kipaumbele. Lazima tufunge mabao na kushinda mechi sio tu kuwa timu bora kila mechi.”

Chelsea wana mechi ngumu kipindi hiki cha sikukuu, kwani watatembelea viongozi wa ligi Arsenal Jumatatu kabla ya kuwa wenyeji wa Swansea City na Liverpool.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC