Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NYAMLANI KUENDELEZA SERA ZA TENGA TFF

Mgombea Urais wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Jumanne Nyamlani amesema endapo atachaguliwa kuliongoza shirikisho hilo lenye mamlaka ya juu kisoka nchini, ataendeleza mambo yote mazuri yaliyofanywa na utawala unaoondoka madarakani chini ya Rais wa sasa, Leodegar Tenga.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Nyamlani ambaye kwa sasa ni makamu wa kwanza wa rais wa TFF, alisema uongozi wa Tenga (58), umefanya mambo mengi mazuri ambayo amepanga kuyaendeleza kwa maslahi ya soka la Tanzania.


"2004 Tenga aliingia madarakani kuchukua uongozi katika shirikisho lililokuwa 'limekufa'. TFF, kipindi hicho iliitwa FAT (Chama cha Soka Tanzania) ilikuwa na madeni, haikuwa na Katiba, lakini katika miaka nane ya uongozi wa Tenga hayo yote yamebaki kuwa historia," alisema Nyamlani na kuongeza:

"Tumeimarisha katiba, sasa tuna katiba bora ya TFF na tumekuwa wazi katika masuala ya mapato na matumizi ya fedha. Tuna kanuni za fedha ambazo hazikuwapo, TFF sasa ni taasisi kubwa yenye wafanyakazi wengi. Nakumbuka 2004 basi la FAT liliuzwa kwa sababu hatukuwa na fedha za kumlipa mmoja wa wafanyakazi wetu."

Nyamlani, ambaye 2008-2012 alikuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Dar es Salaam (DRFA), aliendelea kueleza kuwa katika kuhakikisha Tanzania inapiga hatua kisoka na kushinda mataji makubwa kwenye michuano ya kimataifa, atafanya kazi kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na Shirikisho la Kimataifa la Soka (Fifa).

Alisema ataanza na utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya soka 2003-2006 na baadaye atajikita katika ahadi zake tisa kwa Watanzania ambazo ni kuimarisha usimamizi na menejimenti ya soka katika ngazi zote, kupiga vita rushwa katika soka, kukuza soka la watoto, vijana na wanawake, kuimarisha uwezo wa rasilimali fedha kwa shirikisho, kuongeza ubora na uwezo wa marefa, walimu na wataalam wa afya za michezo.

Zingine ni kuongeza ubora wa Ligi Kuu, Ligi Daraja la Kwanza na ligi za wilaya na mikoa, kuongeza idadi ya mawakala wa wachezaji, kuimarisha ushirikiano wa TFF na serikali na kuwa na uhusiano mzuri na mashirikisho ya Kimataifa, CAF na Fifa.

"Nitaendeleza misingi ya utawala bora ambayo Tenga anatuachia.

Hatukuwa na kamati za kuwaadhibu watu wanaojihusisha na rusha kwenye soka. Tulikuwa tunalazimika kuwashirikisha Takukuru, lakini sasa vyombo hivyo vipo na tutakuwa tunawaadhibu mara moja na kwa haraka zaidi," alisema.

"Utulivu na uwazi uliojengwa na Tenga TFF umetusaidia kupata wadhamini wengi.

TBL wanatoa Sh. bilioni 3.5 kudhamini timu ya taifa. Azam TV nao wamejitokeza na kutoa fungu nono (Sh. bilioni 5.6) kudhamini matangazo ya Ligi Kuu. Ni kwa sababu ya utawala bora wa Tenga na uwazi tunaouonyesha TFF," aliongeza Nyamlani.

Uchaguzi Mkuu wa TFF, ambao ulitakiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu kabla ya kusimamishwa na Fifa, utafanyika keshokutwa jijini Dar es Salaam huku Nyamlani akichuana na Mwenyekiti wa Chama cha Soka Kagera (KRFA), Jamal Malinzi kuwania kumrithi Tenga katika nafasi ya urais.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...