Pigo jingine limeikumba klabu ya Yanga baada ya nyumba anayoishi kiungo wao wa kimataifa Mnyarwanda Haruna Niyonzima 'Fabregas' iliyopo Magomeni Makuti jijini Dar es Salaam kuungua moto jana na kusababisha hasara kubwa.
Niyonzima, ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika kikosi cha Yanga kinachonolewa na kocha Mholanzi Ernie Brandts, alikosa mazoezi ya timu hiyo jana kwenye uwanja wa shule ya sekondari Loyola uliopo Mabibo jijini Dar es Salam kufuatia tukio hilo.
Baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh alisema: "Niyonzima hajafika mazoezini kutokana na kuungua kwa nyumba anayoishi. Lakini taarifa zaidi anazo Kizuguto."
Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema nyumba anayoishi kiungo huyo 'fundi' iliungua lakini hakuwa na taarifa za kina kuhusu balaa hilo.
Mwandishi alikwenda hadi nyumbani kwa Niyonzima ambako alimkuta nahodha huyo wa timu ya taifa ya Rwanda (Amavubi) akiwa amekaa nje ya nyumba hiyo huku uso wake ukionyesha kujawa na huzuni.
Niyonzima alisema moto umeunguza eneo la sebuleni la nyumba hiyo ambayo yeye ni mpangaji na kuteketeza vifaa vyote vilivyokuwapo zikiwamo skrini iliyokua imefungwa ukutani, redio (music system), makochi na samani nyingine za mamilioni ya shilingi.
"Ilikuwa saa inakaribia saa moja asubuhi nikiwa nimepumzika na familia yangu. Nikasikia mtu anatuamsha. Nilipofungua mlango, nikakutana na moshi mzito, sebuleni kwangu kulikuwa kunaungua," alisema Niyonzima.
Akizungumzia tukio hilo, Rabia Abeid, jirani wa Niyonzima, alisema aliona moshi mkubwa unafuka kutoka kwenye sebule ya nyota huyo tegemeo wa Yanga, hivyo kukimbia kwenda kuwaamsha.
Mke wa Niyonzima, Uwineza Naillah, alisema tukio hilo limeitia hasara kubwa familia yao na mmiliki wa nyumba hiyo kwa kuwa atalazimika kuweka madirisha mapya ya vioo na kufanyia ukarabati chumba huku wao wakilazimika kununua vifaa vipya vya sebuleni.
Niyonzima aliendelea kueleza kuwa baada ya kuona hali hiyo walipiga kelele ambazo zilijaza umati wa watu hasa majirani zao ambao walijitokeza kusaidia kuzima moto huo ambao pengine ungesababisha athari kubwa zaidi.
"Nyumba hii ina vyumba vitatu ninavyooishi mimi na familia yangu. Moto ulikuwa umetanda chumbani.
Majirani walijitokeza na kuanza kutusaidia kuzima moto huo kwa kuvunja madirisha ya vioo na kumwaga maji. Mpaka sasa hatujajua chanzo ni ni lakini tumeagiza fundi wa umeme aje aangalie kama moto huo umesababishwa na umeme," alisema Niyonzima.
"Nashukuru tulifanikiwa kuuzima moto lakini vitu vyote vilivyokuwa ndani hatukufanikiwa kuivitoa vikiwa salama. Akili yangu kwa sasa haiko sawa, sikumbuki thamani ya vitu vilivyokuwamo lakini haipungui Sh. milioni tano," alisema zaidi Niyonzima.
Kutokana na tukio hilo, Niyonzima alisema kuna uwezekano mkubwa wa kutoonekana uwanjani na huenda akakosa mechi ijayo dhidi ya mabingwa wa mwaka 1999 na 2000 wa Tanzania Bara, Mtibwa Sugar itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumapili.
Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema uongozi wa umezipokea kwa mashtuko taarifa za kuungua kwa nyumba anayoishi nyota wao na kwamba wanaangalia namna ya kumsaidia.
"Tutaangalia namna ya kumsaidia kutokana na tatizo hilo, lakini msaada wetu utakuwa siri yake na klabu ya Yanga," alisema Mwalusako.
Niyonzima, ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika kikosi cha Yanga kinachonolewa na kocha Mholanzi Ernie Brandts, alikosa mazoezi ya timu hiyo jana kwenye uwanja wa shule ya sekondari Loyola uliopo Mabibo jijini Dar es Salam kufuatia tukio hilo.
Baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh alisema: "Niyonzima hajafika mazoezini kutokana na kuungua kwa nyumba anayoishi. Lakini taarifa zaidi anazo Kizuguto."
Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto alisema nyumba anayoishi kiungo huyo 'fundi' iliungua lakini hakuwa na taarifa za kina kuhusu balaa hilo.
Mwandishi alikwenda hadi nyumbani kwa Niyonzima ambako alimkuta nahodha huyo wa timu ya taifa ya Rwanda (Amavubi) akiwa amekaa nje ya nyumba hiyo huku uso wake ukionyesha kujawa na huzuni.
Niyonzima alisema moto umeunguza eneo la sebuleni la nyumba hiyo ambayo yeye ni mpangaji na kuteketeza vifaa vyote vilivyokuwapo zikiwamo skrini iliyokua imefungwa ukutani, redio (music system), makochi na samani nyingine za mamilioni ya shilingi.
"Ilikuwa saa inakaribia saa moja asubuhi nikiwa nimepumzika na familia yangu. Nikasikia mtu anatuamsha. Nilipofungua mlango, nikakutana na moshi mzito, sebuleni kwangu kulikuwa kunaungua," alisema Niyonzima.
Akizungumzia tukio hilo, Rabia Abeid, jirani wa Niyonzima, alisema aliona moshi mkubwa unafuka kutoka kwenye sebule ya nyota huyo tegemeo wa Yanga, hivyo kukimbia kwenda kuwaamsha.
Mke wa Niyonzima, Uwineza Naillah, alisema tukio hilo limeitia hasara kubwa familia yao na mmiliki wa nyumba hiyo kwa kuwa atalazimika kuweka madirisha mapya ya vioo na kufanyia ukarabati chumba huku wao wakilazimika kununua vifaa vipya vya sebuleni.
Niyonzima aliendelea kueleza kuwa baada ya kuona hali hiyo walipiga kelele ambazo zilijaza umati wa watu hasa majirani zao ambao walijitokeza kusaidia kuzima moto huo ambao pengine ungesababisha athari kubwa zaidi.
"Nyumba hii ina vyumba vitatu ninavyooishi mimi na familia yangu. Moto ulikuwa umetanda chumbani.
Majirani walijitokeza na kuanza kutusaidia kuzima moto huo kwa kuvunja madirisha ya vioo na kumwaga maji. Mpaka sasa hatujajua chanzo ni ni lakini tumeagiza fundi wa umeme aje aangalie kama moto huo umesababishwa na umeme," alisema Niyonzima.
"Nashukuru tulifanikiwa kuuzima moto lakini vitu vyote vilivyokuwa ndani hatukufanikiwa kuivitoa vikiwa salama. Akili yangu kwa sasa haiko sawa, sikumbuki thamani ya vitu vilivyokuwamo lakini haipungui Sh. milioni tano," alisema zaidi Niyonzima.
Kutokana na tukio hilo, Niyonzima alisema kuna uwezekano mkubwa wa kutoonekana uwanjani na huenda akakosa mechi ijayo dhidi ya mabingwa wa mwaka 1999 na 2000 wa Tanzania Bara, Mtibwa Sugar itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumapili.
Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema uongozi wa umezipokea kwa mashtuko taarifa za kuungua kwa nyumba anayoishi nyota wao na kwamba wanaangalia namna ya kumsaidia.
"Tutaangalia namna ya kumsaidia kutokana na tatizo hilo, lakini msaada wetu utakuwa siri yake na klabu ya Yanga," alisema Mwalusako.