Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TFF YAZITUHUMU YANGA, MBEYA CITY KUENDEKEZA USHIRIKINA



Vitendo vivyoashiria imani za kishirikina ambavyo vilidaiwa kujitokeza katika mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Mbeya City dhidi ya Yanga, vimeziponza timu hizo.


Kabla ya kuanza kwa mechi hiyo iliyopigwa Jumamosi katika dimba la Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya na kumalizika kwa sare ya bao 1-1, yaliokotwa mayai katikati ya uwanja na kisha kukabidhiwa kwa meneja wa uwanja huo, Modestus Mwaluka.

Akizungumza katika mahojiano maalum jijini Dar es Salaam jana, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Boniface Wambura (Pichani) , alisema wameshaikabidhi ripoti ya kamishna na ya waamuzi kwa kamati husika kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi.

"Kwa sasa sekretarieti ya TFF haiwezi kuzungumzia suala hilo kwa sababu bado halijapitiwa na kamati husika. Tumepokea ripoti za waamuzi na kamishna wa mechi na kuikabidhi kwa kamati husika," alisema Wambura.

"Tukio hilo liko chini ya TFF kwa sababu ndiyo inayohusika na mambo yote yanayojitokeza ndani ya uwanja.

"Tusubiri maamuzi ya kamati husika. Wao ndio wataamua kulingana na kilichomo kwenye ripoti za maafisa wa TFF waliokuwa wametumwa kusimamia mechi hiyo," alisisitiza Wambura huku akikataa kubainisha timu itakayokumbwa na rungu hilo.

Kwa mujibu wa Kanuni ya 32(1) ya Ligi ya TFF, inakataza klabu kujihusisha na vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina.

"Klabu ina wajibu na jukumu la kuhakikisha kuwa wachezaji, viongozi, wanachama na wapenzi wake wanajiheshimu na hawajihusishi na vitendo vyovyote vya utovu wa nidhamu kama vile matusi, vitisho, vurugu, vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina na vitendo vyovyote vingine visivyokuwa vya kimichezo," inaeleza kanuni hiyo.

Kanuni hiyo inaendelea kuainisha kuwa: "Klabu ambayo mashabiki wake watafanya vitendo hivyo, itatozwa faini ya Sh. 500,000 huku shabiki atakayethibitika kujihusisha na vitendo hivyo, akifungiwa kuingia uwanjani kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu na kisichozidi mwaka mmoja."

Wakati Yanga na Mbeya City zikisubiri kamati ikae kutoa maamuzi, Klabu ya Simba imeponea chupuchupu kukumbana kuingia katika mkumbo huo, kwani nayo ilidaiwa kufanya vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina katika mechi yao ya pili ya ligi hiyo ambayo walishinda 1-0 dhidi ya Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Agosti 28, kabla ya kuanza kwa mechi hiyo iliyokuwa ya kwanza kwa Simba kupata ushindi msimu huu baada ya kushikwa kwa sare ya 2-2 dhidi ya Rhino Rangers mjini Tabora, ilidaiwa walimwaga maji yenye rangi nyekundu chini ya mlango wa basi lao wakati wachezaji wao walipokuwa wakishuka kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.

"Kamati inatolea maamuzi mambo ambayo yamo kwenye ripoti za kamishna na marefa tu. Tukio la ushirikina linalodaiwa kufanywa na Simba jijini Arusha halikuwamo kwenye ripoti zao. Kamati haiwezi kukaa kuzungumzia suala ambalo halina ushahidi," alisema Wambura.

Rufaa  ya Yanga yatupwa

Katika hatua nyingine, TFF imeitupilia mbali rufani iliyowasilishwa na Yanga kuomba kurudiwa kwa mechi yao dhidi ya Mbeya City kwa madai ya kujitokeza kwa vurugu uwanjani.

Jumapili uongozi wa Klabu ya Yanga ulisema umewasilisha rufaa TFF kwa njia ya barua pepe kwa Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Angetile Osiah kuomba mechi hiyo irudiwe katika uwanja huru kutokana na vurugu zilizotokea kabla ya mechi hiyo.

"TFF inashughulikia matukio ambayo yanatokea ndani ya uwanja tu. Vurugu za mashabiki nje ya uwanja na suala la magari ya Yanga kupigwa mawe ni ya polisi, hatuwezi kuita kamati kuzungumzia mambo ambayo hayapo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC