Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAMBWE KUIBUKIA YANGA OKTOBA 20

Mshambuliaji mpya wa Simba, Mrundi Amisi Tambwe, 'amewatishia nyau' mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga baada ya kuweka wazi kuwa amejipanga kuwafunga kwenye mechi yao ya kwanza ya ligi kuu itakayopigwa Oktoba 20 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


Baada ya kuifungia Simba bao la pili katika mechi waliyotoka sare ya 2-2 dhidi ya Mbeya City, Tambwe alikwenda karibu na jukwaa la mashabiki wa Yanga na kuwanyooshea kidole, ishara ambayo iliibua maswali mengi kutoka kwa watu waliokuwamo uwanjani hapo kushuhudia mchezo huo.

Bao hilo lilikuwa la pili kwa Tambwe katika mchezo huo na la sita kwake kwenye mechi mbili kwani pia alifunga mabao manne wakati Simba ikishinda 6-0 dhidi ya Mgambo Shooting.

Akizungumza katika mahojiano maalum jijini Dar es Salaam juzi, Tambwe alisema aliamua kuwaonyesha ishara hiyo mashabiki wa Yanga kwa sababu walikuwa wakimzomea kabla ya kufumania nyavu.

"Nimejiunga na Simba nikijua kwamba wapinzani wao wakubwa ni Yanga. Walitumia muda wao kunizomea kabla ya kufunga. Na hata nilipofunga bao la kwanza waliendelea kunizomea. Najipanga kuhakikisha ninaifunga timu hiyo tutakapocheza nayo," alisema Tambwe.

Mrundi huyo aliyetua Simba msimu huu baada ya kuipa Klabu ya Vital'O ubingwa wa Ligi Kuu Burundi pamoja na Kombe la Kagame, kwa sasa anaongoza kwa ufungaji katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara akiwa na mabao sita.

Tambwe, ambaye amecheza dakika zote 360 katika mechi nne ambazo vinara wa msimamo huo, Simba walizocheza dhidi ya Oljoro JKT, Mtibwa Sugar, Mgambo na Mbeya City, hakufunga katika mechi mbili mfululizo.

Mechi ambazo hakufunga ni wakati wakishinda 1-0 ugenini dhidi ya Oljoro JKT na 2-0 nyumbani dhidi ya mabingwa wa 1999 na 2000 Mtibwa Sugar.

Kadhalika Tambwe ambaye ni mfungaji bora wa Kombe la Kagame msimu huu, hakucheza mechi ya ufunguzi waliyong'ang'aniwa kwa sare ya 2-2 dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora baada ya yeye na Mrundi mwenzake, Gilbert Kaze kuzuiwa na Shirikisho la Soka nchini(TFF) kutokana na kuchelewa hati zao za Uhamisho wa Kimataifa (ITC).

Msimu uliopita katika Ligi Kuu ya Burundi, Tambwe aliibuka mfungaji bora baada ya kufunga mabao 21 katika mechi 18, na baadaye kufanya hivyo tena kwa kufumania nyavu mara sita kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika mjini Darfur, Sudan na Vital'O kutwaa ubingwa.

Mrundi huyo anatajwa kuwa mrithi sahihi wa Mganda Emmanuel Okwi ambaye aliuzwa kwa Klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia msimu uliopita, jambo ambalo lilichangia Simba kupoteza ubingwa kwa mahasimu wao wa jadi, Yanga.

Okwi na benchi la Ufundi la Yanga likiongozwa na kocha wao, Mholanzi Ernie Brandts walikuwapo uwanjani Jumamosi wakati Tambwe akidhihirisha makali yake kwa kufunga mabao mawili kwenye mechi hiyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC