Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STEWART HALL KUTIMULIWA AZAM, MOROCCO, BANYAI NAO KUTUPIWA VIRAGO

Hali si shwari! Vibarua vya makocha watatu Hassan Banyai wa Ashanti United, Hemed Morocco wa Coastal Union na Stewart Hall wa Azam vipo katika hatihati kutokana na mwenendo mbovu wa timu zao katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara.


Ashanti United imetangaza kumsimamisha kocha wake Banyai ikiwa ni mwezi mmoja tangu walipoingia naye mkataba wiki moja kabla ya kuanza kwa ligi Agosti 24.

Katibu wa Ashanti United, Abubakari Silas alithibitisha kuwa klabu hiyo imemsimamisha Banyai na hayupo katika kikosi kilichokwenda Kagera kuivaa Kagera Sugar na jana hakuwapo katika mechi ya juzi wakati Ashanti ilipocheza dhidi ya Azam.

Naye meneja wa Ashanti, Mbaraka Hassan alisema wameamua kumsimamisha kocha huyo kufuatia matokeo mabaya ya timu, ambapo kikosi hicho kitakuwa chini ya kocha msaidizi Hassan Ibrahim.

“Kwa sasa kuanzia mchezo wetu na Azam timu ilikuwa chini ya kocha msaidizi baada ya mapendekezo ya uongozi kumsimamisha kwa muda Banyai, siyo kama amefukuzwa bali tunafuatilia kwa ukaribu maendeleo ya timu, atarudishwa wakati wowote uongozi utakapoafikiana,” alisema Mbaraka.

Kocha Banyai hakuwapo kwenye benchi wakati Ashanti ikipata pointi yake ya kwanza msimu huu baada ya kulazimisha sare 1-1 na Azam kwenye Uwanja wa Chamazi uliopo nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Upepo huo mbaya umepita, pia kwa Azam ambayo lengo lao la kutwaa ubingwa limeanza kwenda kombo baada ya mechi nne ilizocheza kwenye ligi na kushinda moja tu dhidi ya Rhino Rangers na kuambulia sare tatu dhidi ya Ashanti United, Mtibwa Sugar, Kagera Sugar na kushika nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi sita.

Uongozi wa timu hiyo umekasirishwa na matokeo hayo na juzi waliitisha kikao cha dharura na kocha Hall kujadili mwenendo huo.

Baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ashanti, kocha Stewart Hall alikataa kuzungumza na gazeti hili akisema,”nawahi kwenye kikao, kwa sasa sina muda wa kuzungumza na mwandishi.”

Jitihada zilizofanywa kufuatilia kilichojiri kwenye kikao hicho cha dharura ziligonga mwamba baada ya simu za viongozi wa klabu kuita bila kupokelewa.

Ingawa Ofisa habari wa Azam FC, Jafar Iddi alipatikana kwenye simu, lakini aligoma kusema lolote na kujitetea kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu kuwa yuko darasani hawezi kupokea simu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...