Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YAINGIA MCHECHETO, YATISHWA NA KASI YA MBEYA CITY

Timu ya Mbeya City ambayo imepanda daraja la ligi kuu ya Bara kwa mara ya kwanza katika historia yake mwaka huu inaweza kuwa inalingana kwa pointi na mabingwa watetezi Yanga ambao waliilazimisha kutoka sare ya 1-1 wiki iliyopita, lakini inakutana na mtihani wake mgumu zaidi leo itakapokuwa mgeni wa Simba kwenye Uwanja wa Taifa.


Tangu ianze kucheza kwa mara ya kwanza ligi kuu mechi nne zilizopita, City haijafungwa ikiwa na pointi sita zilizotokana na sare tatu na ushindi katika mchezo mmoja -- kama Yanga.

Lakini inaikabili Simba leo katika mchezo wake wa pili tu ugenini huku mabingwa hao wa mwaka jana wakiwa wenye ari kubwa iliyotokana na ushindi mkubwa wa mabao 6-0 dhidi ya Mgambo JKT kwenye uwanja huo, katikati ya wiki.

Kupata ushindi mkubwa zaidi katika msimu huku mshambuliaji wake tegemeo Amisi Tambwe akifikia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi katika mechi moja ya ligi kuu ni mazingira ambayo yangeweza kuifanya Simba ipoteze umakini inapokutana na City.

Lakini bahati mbaya kwa wageni hao wa ligi kuu, kocha msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu amesema timu yake haijabweteka kwa ushindi wake wa kishindo.

Akizungumza jana, Kihwelu alisema hata kuifunga Mgambo hakujawathibitishia kuwa wana kikosi bora kuliko timu nyingine kwenye ligi hiyo, ikiwemo City, hivyo wataikabili kwa uzito sawa na mechi nyingine.

"Sisi tunaendelea kujipanga, kama benchi la ufundi kila mchezo kwetu tunauchukulia katika uzito sawa bila kuangalia tunacheza na nani," alisema.

"Tumejiandaa kuwakabili kwa nguvu zote Mbeya City kwa sababu ni moja ya timu nzuri kwenye ligi. Hatutawadharau kamwe."

Alisema anaifahamu City kama timu yenye kikosi kilichokaa pamoja kwa muda mrefu na hivyo matokeo inayopata hayamshangazi.

Mbali na sare dhidi ya Yanga, City ilipata matokeo hayo dhidi ya Kagera Sugar na Coastal Union na kuifunga Ruvu Shooting 2-1.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC