Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NGASA AITANGAZIA VITA SIMBA, AAPA KUILIZA OKTOBA 20

Winga Mrisho Ngasa (Pichani) wa Yanga amesema ataendelea kucheza kwa kujituma zaidi ili kukisaidia kikosi chake hicho kipya kufikia malengo na kuweka wazi kwamba amejipanga kuifanyia 'kitu mbaya' Simba katika mechi yao ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara itakayochezwa Oktoba 20.


Ngasa alilazimika kuwalipa Simba Sh. milioni 45 (Sh. milioni 30 alizochukua ili kusaini kuichezea klabu hiyo na Sh. milioni 15 za fidia), jambo lililofanya licha ya kuitumikia bado "imekula kwake" na Simba ndiyo iliyonufaika.

Wakati akiendelea kuuguza machungu ya kulipa mamilioni hayo, Ngasa anataka kufidia maumivu yake dhidi ya Simba kwa kutumia mpira uwanjani.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mechi yao ya juzi waliyoshinda 1-0 dhidi ya 'maafande' wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana, Ngasa alisema kuwa ana deni kwa mashabiki wa Yanga, hasa baada ya kukosa mechi sita za timu yao ikiwamo ya Ngao ya Hisani walioshinda 1-0 dhidi ya Azam na tano za ligi kuu baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka (TFF).

Ngasa, ambaye juzi alitoka kifungoni na kutoa pasi ya mwisho ya goli pekee la mechi lililofungwa na mshambuliaji Mganda Hamis Kiiza, alisema anaisubiri kwa hamu mechi yao dhidi ya Simba ili 'kumaliza hasira zake' za zilizotokana na kuamuliwa kulipa mamilioni ya fedha.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ilimfungia mechi sita mzaliwa huyo wa jiji la Mwanza na kumtaka alipe Sh. milioni 45 baada ya kubaini kuwa aliingia mkataba na Simba kwa ajili ya kuitumikia il-hali bado alikuwa na mkataba na Azam.

Hata hivyo, hukumu hiyo ililalamikiwa kwamba ilitolewa kisiasa kwa maelezo kwamba Simba pia ilipaswa kuadhibiwa kwa kuhusika katika jambo hilo, kwa kumsainisha mkataba mchezaji ambaye ilitambua kuwa alikuwa bado ana mkataba na timu nyingine wakati walipomchukua kwa mkopo wa mwaka mmoja kutoka Azam.

Baada ya kutoa pasi ya goli la ushindi juzi, Ngasa alikwenda jirani na jukwaa la Simba na kuanza kuwapungia mikono 'Wanamsimbazi', ishara ambayo alisema kuwa inamaanisha ameanza kazi na wajiandae kwa kipigo Oktoba 20.

"Nina deni kubwa kwa mashabiki wa Yanga, namshukuru Mungu nimemaliza adhabu na leo (juzi) nimetoa pasi ya goli... Simba wajiandae tutakapokutana nao tutawaonyesha kazi," alisema Ngasa ambaye katika mechi ya juzi alicheza vizuri licha ya kuwa nje ya uwanja tangu kuanza kwa ligi hiyo inayodhaminiwa na Vodacom Agosti 24.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...