Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: SUGU, KAIMBE MUZIKI, MJENGONI HAKUKUFAI.........

LUCKY Dube alikuwa Mwanaharakati wa uhuru nchini Afrika Kusini, Dube (Marehemu) alipigania uhuru wa nchi hiyo iliyokuwa ikitawaliwa kimabavu na makaburu.


Makaburu waliendesha kampeni yao ya ubaguzi wa rangi iliyopelekea mauaji kwa wazalendo wa nchi hiyo ambao wengi wao walikuwa watu weusi, walibaguliwa vya kutosha.

Muziki wa reggae ulitumika kama sehemu ya kufikisha ujumbe kwamba wazalendo wanateseka na sasa waachiwe huru, Mwaka 1990 Nelson Mandela aliruhusiwa kutoka kifungoni ambapo alihukumiwa kwenda jela maisha ili kuwatetea wazalendo.

Baadae Afrika Kusini ikawa huru, safari za Watanzania kwenda `Sauzi`au Bondeni kama wanavyoita zikaanza kuongezeka lakini ukitaja orodha ya wanaharakati wa ukweli waliojitoa kwa nguvu zao hadi kupatikana uhuru kamili Lucky Dube ni miongoni mwao.

Orodha hiyo pia inawataja Miriamu Makeba,Ivonne Chakachaka na wengineo wengi  ambao wanaeshimika, lakini cha kushangaza wote hao hawakuwahi kuthubutu kugombea ubunge wala udiwani.

Wameishia kuimba muziki na heshima wakaipata tena ulimwengu mzima unawatambua, Tanzania haikupitia shuruba kama ilizopitia Afrika Kusini,labda Watanzania waliduwazwa kwa kunyimwa Elimu, maana wakati wa Baba wa Taifa marehemu Mwl Julias Kambarage Nyerere akienda UN kuomba uhuru, nchi yetu ilikuwa na wasomi 7 tu.

Kwa sasa nchi yetu tayari iko huru, fulsa tu ndizo zinazohitajika kutumiwa vema lakini kuna kundi kubwa la watu wanaojiita wanaharakati tena wana misimamo mikali.

Joseph Mbilinyi a k a Sugu au Mr 11 ni miongoni mwa wanaharakati waliopo hapa nchini, Sugu alianza kujiingiza kwenye harakati pale alipoanza kuimba muziki wa kufokafoka maarufu Rap.

Muziki huo ulianza kushamili hapa nchini katika miaka ya 90 ambapo vijana wengi walikita, licha kwamba ulionekana wa kihuni lakini ukaja kukubalika ndipo Mr 11 alipoanza kung'ara.

Ingawa katika tungo zake hakuwahi kuipinga serikali wala kuonyesha hisia kwamba ni mwanaharakati, isipokuwa ameonekana kama mwanaharakati kutokana na hisia zake.

Tungo zake nyingi ziliusiana na mapenzi, majisifu nakufurahi, Aliyekuja kuonekana mwanaharakati wa waziwazi ni msanii mwenzake Joseph Haule`Profesa Jay`.

Jay aliimba nyimbo zilizonyesha kupinga baadhi ya tabia za wanasiasa ambao huomba kura ili kuongoza kwa kusema uongo, Lakini Sugu ndiye msanii aliyepata mafanikio pengine kuliko msanii yeyote hapa nchini.

Aliweza kufyatua album tano mfululizo na enzi yake hakuwa na mshindani, ziara yake nchini Marekani ilianza kumjenga zaidi na kuitangaza Tanzania kimataifa.

Akiwa Marekani Sugu alizindua album yake ya sita iliyojulikana kwa jina la 'Deiwaka', baadae alikuja na mipango mizuri ya kuanzisha kampuni yake ya kusaidia wanamuziki chipukizi.

Kampuni hiyo ilifahamika kwa jina la 'Deiwaka Production' ambapo pia ilikuwa na wazo la kuanzisah kampeni ya kupambana na malaria iliyofahamika kwa 'Malaria haikubaliki' ambayo baadaye ilileta kizaazaa baina yake na Cloud`s Media iliyopo chini ya Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba.

Sitaki kuelezea ugomvi wake na Ruge kwani walifikia pabaya mpaka nyimbo za matusi zilitungwa, Ila Sugu akajitosa rasmi kwenye harakati za kutaka kuking'oa chama tawala madarakani.

Sugu alijiingiza kwenye ulingo wa siasa na akajiunga na chama chenye ushawishi mkubwa wa nguvu ya umma (CHADEMA) na moja kwa moja akateuliwa kluwa mgombea ubunge Mbeya mjini.

Chama hicho kwa kutambua heshima aliyonayo Sugu kwenye muziki kama ilivyo kwa Lucky Dube wa Afrika Kusini ikamkabidhi jimbo la Mbeya mjini kuwania Ubunge.

Hakupata upinzani akafanikiwa kumbwaga mpinzani wake ambaye alikuwa  mwanachama wa chama tawala CCM, kwa heshima aliyonayo Sugu ni lazima apate ushindi, Sugu ndiyo aliemuinua kimuziki Afande Sele, Stara Thomas na Lady Jay Dee si mtu wa masihara hata kidogo.

Lakini alipofanikiwa kuingia 'Mjengoni' ameshindwa kung'ara kama alivyokuwa aking'ara kwenye muziki.

Sijaona makali ya Sugu kwenye pale 'mjengoni' kama ilivyokuwa kwenye muziki, cha zaidi nimeona fedheha dharau kwa mheshimiwa huyo nilimuhusudu sana enzi za `Mambo ya fedha, Dar DSM na Deiwaka.

Sugu amedhalilishwa mno pale kikosi cha usalama bungeni walivyotumia maguvu yao kumkwida na kumpiga kama kibaka au mtumiaji wa dawa za kulevya`Teja.

Heshima yote aliyokuwa nayo na uheshimiwa wake kutokana na siasa ilikuwa kazi bure. Nikiwa kama shabiki wake kwenye muziki namuomba arejee kwenye tasnia yake ya muziki, kule `Mjengoni akumfai.

Tanzania tunafanya siasa baridi hakuna haja ya kugombana kama ilivyotokea hivi karibuni ambapo wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kuzichapa kavukavu. Tuonane wiki ijayo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...