Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KOCHA AZAM AWATAJA WACHAWI WAKE.........

Kocha Stewart Hall (Pichani) amesema alimuacha nje ya kikosi cha kwanza cha Azam mfungaji bora wa ligi msimu uliopita, Kipre Tchetche na kiungo bora yosso Salum Aboubakar 'Sure Boy', katika mechi waliyoshinda 3-2 dhidi ya mabingwa Yanga, kwa sababu nyota hao wanaonekana wameridhika na mafanikio ya msimu uliopita na hawajitumi.


"Kuwa na mafanikio msimu uliopita hakukuhakikishii mafanikio msimu huu," alisema Hall.
Muingereza huyo aliongeza kuwa sare tatu katika mechi nne zilimfadhaisha na aliona kuna tatizo kikosini kwamba baadhi ya wachezaji wanaotegemewa hawajitumi.

"Ndiyo maana nikaamua kuwachezesha yosso na nikawaacha nje Kipre Tchetche na Sure Boy. Wanapaswa kujituma ili kuendelea kupata namba kikosini. Niliwaanzisha vijana kwa sababu najua wana usongo wa kupata mafanikio, wanajituma. Huwezi kucheza kama huna bidii," alisema Hall.

Imani yake kwa yosso ilimlipa Hall, ambaye aliwashuhudia wachezaji waliopandishwa kutoka timu yao ya vijana, winga Farid Musa na mshambuliaji Joseph Kimwaga waking'aa.

Kimwaga (18), ambaye aliingia katika uwanjani katika dakika ya 72 kuchukua nafasi ya yosso mwenzake, Musa, aliifungia Azam goli la ushindi katika dakika ya mwisho ya mchezo.

Matokeo hayo yalizima uteja wa Azam wa mechi nne mfululizo kutoka kwa Yanga, ambayo ilitawala kiasi kikubwa cha mechi ya juzi.

Hall pia aliisifu Yanga kuwa ilicheza vizuri zaidi yao akisema kwamba "timu bora" haikushinda juzi baada ya kuwashuhudia mabingwa hao watetezi wakikosa bahati baada ya mashuti yao  mawili kugonga mwamba, huku kipa wa Wanalambalamba, Aishi Manula akifanya kazi ya ziada kuzuia "mvua" ya magoli langoni mwa Azam.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC