Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIPSANG AVUNJA REKODI YA BERLIN MARATHON

Mkenya Wilson Kipsang amevunja rekodi ya dunia ya mbio za Marathon kwa kupunguza sekunde 15 aliposhinda mbio za Berlin mapema jumapili.


Mkimbiaji huyo mwenye umri wa miaka 31 aliandikisha mda wa saa mbili dakika tatu na sekunde 23 kuondoa rekodi ya zamani iliyowekwa na Mkenya mwenzake Patrick Makau miaka miwili iliyopita.

Rekodi hiyo iliwekwa katika mji mkuu wa Ujerumani ambako Makau alikimbia kwa mda wa saa 2:dakika 03:na sekunde 38.
Wilson Kipsang

Kipsang katika mitaa ya Berlin

Wakenya wengine walioshiriki mbio a Berlin Eliud Kipchoge alimaliza katika mda wa saa 2:04:05) huku Geoffrey Kipsang akiweka mda wa saa 2:06:26 katika nafasi ya tatu.

Makau hakushiriki mbio hizi baada ya kujiondoa wiki mbili zilizopita kutokana na kuuguza jeraha la goti.

Wilson alifanya mazowezi akiwa na nia ya kuvunja rekodi ya Berlin na moja kwa moja alianza mbio za leo kwa kudhibiri uongozi katika hatua ya kilomita 10 za mwisho, akiwaacha wenzake walioonekana kuishiwa na pumzi ya kumkimbiza.

Baada ya mbio hizi Kipsanga alisema," Nimefurahi sana kwa ushindi huu na kwa kuvunja rekodi,"

"nilivutiwa mno na Paul Tergat wakati akikimbia na kuvunja rekodi hii miaka kumi iliyopita katika mashindano haya haya.

Ushindi wa Kipsang unampa jumla ya ushindi wa saba tangu aanze kushiriki mashindano ya marathon mjini Paris,Ufaransa miaka mitatu iliyopita.

Itakumbukwa kuwa Kipsang alishinda mbio za marathon za London mwaka jana na kwenye michezo ya Olimpiki alimaliza wa tatu na kujishindia medali ya fedha mjini London.

Ushindi wa mbio hizi za Berlin ni wa kwanza mwaka huu. Licha ya mbio za London kua mojapo ya mbio muhimu duniani na kwake aliweza kumaliza wa tano mapema mwezi Aprili mwaka huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC