Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HATIMAYE HAPPYNESS AMVUA TAJI BRIGITE

Happiness Watimanywa (19) (Pichani) ameung'arisha mkoa wa Dodoma na Kanda ya Kati usiku wa kuamkia jana wakati alipotwaa taji la urembo la taifa 'Redd's Miss Tanzania 2013' baada ya kuwashinda warembo wengine 29 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.


Mrembo huyo ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Strathclyde kilichoko Glassgow, Scotland anayesomea digrii ya biashara anakuwa wa pili kutoka Dodoma kutwaa taji hilo baada ya Emily Adolph kuibuka mshindi wa taji hilo katika shindano lililofanyika mwaka 1995.

Nyota ya Happiness kutwaa taji hilo ilianza mapema akiwa kambini kwa kuwa mrembo wa kwanza kuingia hatua ya 15 bora kwa kutwaa taji la Redd's Miss Photogenic na alionekana 'kuwateka' wadau wa sanaa ya urembo kwa kushangiliwa kila alipokuwa anapita jukwaani na mavazi ya aina tatu waliyovaa warembo hao.

Akijibu swali alilochagua kuwa atafanya kitu gani tofauti endapo atashinda taji hilo ambacho hakikufanywa na warembo waliopita Happiness alisema mbali na kufanya kazi za jamii atatumia muda wake kutangaza vivutio vya utalii vyote vilivyoko Tanzania ili kuvutia wawekezaji waje kuwekeza nchini.

Mbali na kuvalishwa taji na mrembo namba mbili wa shindano hilo mwaka jana, Eugine Fabian, Happoness aliyezaliwa Morogoro alipewa zawadi ya gari jipya aina ya Toyota Vitz na jana jioni alitarajiwa kukabidhiwa Sh. milioni nane kutoka kwa wadhamini wakuu Redd's Original.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na Latifa Mohamed kutoka Kigamboni, Kanda ya Temeke ambaye atazawadiwa Sh. milioni 6.2 wakati mshindi wa tatu ni Clara Bayo wa Ilala naye atajinyakulia Sh. milioni nne na Elizabert Pert wa Pwani (Mashariki) ataondoka na tatu huku Lucy Tomeka aliyekamilisha tano bora atazawadiwa Sh. milioni 2.4.

Warembo wengine waliofanikiwa kuingia hatua ya 15 bora ni Narietha Boniface (Redd's Miss Top Model na balozi wa Marie Stopes Tanzania), Prisca Clement (Redd's Miss Talent), Severina Lwinga (Redd's Miss Personality), Jane Awetu, Nicejack Herman, Eshy Rashid, Neema Mality, Doris Mollel, Nancy Moshi na Sabrina Juma.

Washiriki wengine 15 waliobakia ambao ni Anastazia Donald, Lina Allan, Jacquiline Luvanda, Diana Laizer, Sabra Islam, Lucy Charles, Salsha Esdory, Miriam Manyanga, Lucy James, Svetlana Nyamweyo, Glory Minja, Mary Chemponda, Philios George, Alice Isaac na Sarah Martin kila mmoja atapata kifuta jasho cha Sh. 700,000.

WAREMBO JUKWAANI

Shindano la Redd's Miss Tanzania lilianza rasmi saa 4:01 kwa warembo kupanda jukwaani wakiwa wamejigawa makundi matatu kwa kucheza shoo ya ufunguzi ya wimbo uitwao 'Personally' wa kundi la P-Square la Nigeria na kufuatia vazi la ubunifu, ufukweni yaliyobuniwa na Veronica Lugenzi na kumalizia na vazi la usiku.

LADY JAY DEE AFUNIKA

Mshindi wa tuzo ya mwanamuziki bora wa kike wa mwaka, Judith Wambura, maarufu Lady Jay Dee alifanikiwa kuwaimbisha wadau wa sanaa ya urembo waliohudhuria shindano la Redd's Miss Tanzania na kibao chake kinachotamba kiitwacho 'Yahaya'.

Jay Dee alipanda mara mbili jukwaani ambapo awali aliimba nyimbo mbili ukiwamo wa 'Joto Hasira' na aliporejea ndipo aliwasha moto kwa kuimba kibao cha 'Yahaya'.

Hata hivyo mkongwe huyo hakupanda stejini na madansa kama ilivyozoeleka katika siku za hivi karibuni kwa wasanii wa kizazi kipya kupambwa na wacheza shoo wao maalum.

Mganda, Mike Ross, alishindwa kutamba kwenye onyesho hilo huku kikundi kingine kilichotoa burudani kilikuwa ni cha sarakasi na ngoma za asili cha Mama Afrika.

Warembo wote jana jioni walitarajiwa kukabidhiwa zawadi zao za fedha katika sherehe ya kuwaaga na leo asubuhi walivunja kambi rasmi na kurejea katika familia zao.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC