Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BAADA YA KUTOKA SARE MFULULIZO, MGOGORO MKUBWA KUIBUKA YANGA

WANACHAMA na wapenzi wa Yanga SC walioongozana na timu mjini hapa, wameanza kukata tamaa juu ya mwenendo wa timu hiyo katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya sare tatu mfululizo, wakisema mambo mawili makubwa, wachezaji kutojituma na mgawanyiko ndani ya uongozi.


Baada ya sare ya tatu mfululizo ya 1-1 na Prisons mjini hapa jana, kama ilivyokuwa dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Mbeya City Uwanja wa Sokoine mjini hapa, baadhi ya wanachama waliangua kilio uwanjani.

Wakiondoka kinyonge Uwanja wa Sokoine, walikuwa wakiwalaumu wachezaji wao kutojituma, kwamba imesababisha timu kuambulia pointi tatu ndani ya mechi tatu.

Lakini pia walikuwa wakisema, kitendo cha kutengwa kwa mfanyabiashara Seif Ahmad ‘Magari’ nacho kinaweza kuwa kinachangia matokeo hayo.

Wanadai Seif ni rafiki mkubwa wa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu yao- Abdallah Ahmed Bin Kleb, hivyo kumpoteza mmoja wao ni sawa na kuwapoteza wote.

Wamestaajabu Bin Keb kutoonekana katika mechi za karibuni za timu hiyo kwa taarifa za kuwa kwenye safari za kibiashara wakati si kawaida yake na wanahisi hali hiyo kwa kiasi kikubwa inachangia matokeo mabaya.

Wanachama hao wameingiwa hofu pia juu ya mchezo wao ujao dhidi ya Azam FC Jumapili Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwamba nao unaweza kuleta matokeo mabaya.

“Timu iondoke hapa Alhamisi, itafika Dar es Salaam usiku na wachezaji wamechoka. Sasa tazama, Ijumaa na Jumamosi siku mbili tu ujiandae kucheza na Azam?”alihoji Paulina, mmoja wa wanachama waliosafiri na timu kutoka Dar es Salaam.

Yanga SC imeambulia pointi sita tu katika mechi nne za mwanzo wa msimu, ikishinda 5-1 dhidi ya Ashanti United na kufuatiwa na sare tatu mfululizo za 1-1 dhidi ya Coastal, Mbeya City na Prisons.

Baada ya mechi jana kocha wa Yanga SC, Mholanzi, Ernie Brandts hakutaka hata kuzungumza na Waandishi wa Habari, wakati mpinzani wake, Jumanne Chale wa Prisons alisema timu yake ingeweza kushinda kama ingetumia vizuri nafasi ilizozipata.

Chale akawazungumzia Yanga akisema kwamba ni timu inayofungika, kwa sababu katika uchezaji wake inaacha mianya ya wazi ya wapinzani kupita na akajutia sare hiyo.

Jerry Tegete alitangulia kuifungia Yanga SC dakika ya 37 jana akiunganisha krosi maridadi ya winga Simon Msuva kabla ya Michael Peter kuisawazishia Prisons dakika ya 77 akiunganisha krosi ya Omega Seme anayecheza kwa mkopo kutoka Jangwani.
 
Yanga SC ilicheza vizuri zaidi kipindi cha kwanza na kupoteza nafasi mbili nzuri za kufunga mabao zaidi dakika ya tatu, Didier Kavumbangu alipowababatiza mabeki shuti kali baada ya kupokea krosi ya Simon Msuva na Jerry Tegete dakika ya saba aliwatoka vizuri mabeki wa Prisons, lakini akapiga nje.

Kipindi cha pili, Prisons walibadilika nao kuanza kushambulia langoni mwa Yanga na kwa ujumla katika ngwe hiyo timu zilishambuliana kwa zamu na mchezo ulikuwa mkali baada ya matokeo kuwa 1-1.

Yanga walionekana kupigana zaidi kusaka bao la ushindi, lakini Prisons walisimama imara kuzuia na kushambulia pia na dakika ya 87 almanusra Prisons wapate bao la pili baada ya Ibrahim Isihaka kupiga kichwa juu kidogo ya lango kufuatia krosi ya Julius Kwanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC