Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AMISI TAMBWE AZITISHA YANGA, MBEYA CITY

Baada ya kufunga mabao manne katika ushindi wa 6-0 Simba iliyoupata dhidi ya Mgambo JKT juzi, mshambuliaji wa timu hiyo, Mrundi Amisi Tambwe (Pichani) ametamba kuendelea kufumania nyavu Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, ikiwano mechi dhidi ya Yanga.


Tambwe aliyetua Simba msimu huu baada ya kuipa Klabu ya Vital'O ubingwa wa Ligi Kuu Burundi  pamoja na Kombe la Kagame, alisema kinachoendelea sasa ni kazi ya kucheka na nyavu tu.

Akizungumza katika mahojiano maalum baada ya kumalizika mechi dhidi ya Mgambo JKT iliyopigwa Uwanja wa Taifa juzi, Tambwe alisema ilimchukua muda kabla ya kuufahamu vema mfumo wa timu hiyo, lakini sasa haumsumbui tena.

Alisema licha ya kabla ya juzi kocha Abdallah Kibadeni kumchezesha kwa dakika zote 180 wakati wakishinda 1-0 dhidi ya Oljoro JKT Agosti 28, mwaka huu jijini Arusha, na baadaye kuwamo katika kikosi kilichoibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, alikuwa hajaushika vema mfumo wa timu hiyo.

Tambwe ambaye kwa sasa anaongoza kwa ufungaji katika ligi hiyo baada ya kufumania nyavu mara nne, huku akifuatiwa na Jerry Tegete wa Yanga na kiungo wa Simba, Haruna Chanongo wenye mabao matatu kila mmoja, hakucheza mechi ya ufunguzi dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora.

Katika mechi hiyo ya ufunguzi iliyopigwa Uwanja Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora na kumalizika kwa sare ya 2-2, Tambwe na Mrundi mwenzake, Gilbert Kaze walizuiwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) kwa kutokana na kukosa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC).

"Nilikuwa sijazoea mfumo wa klabu yangu (Simba) na ligi ya Tanzania ambayo ni ngumu kuzidi ya kwetu (Burundi). Sasa nimeshazoeana na wachezaji wenzangu ndiyo maana nimefunga mabao haya," alisema Tambwe.

"Nafanya mazoezi kwa kujituma, natumai nitafanya vizuri zaidi katika mechi zinazofuata. Licha ya kuibuka na ushindi mnono, Mgambo ni timu nzuri. Nitaendelea kufanya kazi kwa kujituma zaidi ili pia nifunge katika mechi zinazofuata kwani kwa kufanya hivyo nitawapa raha mashabiki wangu na klabu ya Simba."

Msimu uliopita katika Ligi Kuu ya Burundi, Tambwe aliibuka mfungaji bora baada ya kufunga mabao 21 katika mechi 18, na baadaye kufanya hivyo tena kwa kufumania nyavu mara sita kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyofanyika mjini Darfur, Sudan na Vital'O kutwaa ubingwa.

Mrundi huyo anatajwa kuwa mrithi sahihi wa Mganda Emmanuel Okwi ambaye aliuzwa Klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia msimu uliopita, jambo ambalo lilichangia Simba kupoteza ubingwa kwa mahasimu wao wa jadi, Yanga.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC