Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ABEL DHAILA AMSUTA JUMA KASEJA

KIPA Mganda wa Simba SC, Abbel Dhaira ameonekana kuimarika baada ya kudaka mechi tatu mfululizo bila kuruhusu hata bao moja katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara- hali ambayo inaweza kuwafanya wapenzi wa timu hiyo wasahau kuhusu Juma Kaseja.


Dhaira alikuwa ana mwanzo mbaya ndani ya Simba SC, akifungwa mabao 18 katika mechi 11 alizoidakia klabu hiyo tangu Januari mwaka huu alipojiunga nayo hadi Agosti 24, hali ambayo iliibua tetesi za klabu hiyo kutaka kumrejesha kipa wake wa muda mrefu, Kaseja iliyemtema mwishoni mwa msimu.

Lakini baada ya kufungwa mabao mawili rahisi katika sare ya 2-2 na Rhino Rangers Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora, Dhaira aliyetua Msimbazi akitokea IBV ya Ligi Kuu ya Iceland, amedaka mechi tatu bila kuruhusu nyavu zake kutikiswa, Simba ikishinda 1-0 dhidi ya JKT Oljoro mjini Arusha, 2-0 na Mtibwa Sugar na jana 6-0 na Mgambo JKT, Dar es Salaam.
 
REKODI YA DHAIRA TANGU ATUE SIMBA

Simba SC 1-1 Bandari (Kombe la Mapinduzi, alifungwa moja)
Simba SC 0-1 U23 Oman (Kirafiki, alifungwa moja)
Simba SC 1-3 Qaboos (Kirafiki, alidaka nusu akafungwa mawili)
Simba SC 0-4 R. de Libolo (Ligi ya Mabingwa, alifungwa manne)
Simba SC 2-1 Coastal Union (Ligi Kuu, alifungwa moja)
Simba SC 2-2 Azam FC (Ligi Kuu, alifungwa mbili)
Simba SC 1-0 Kahama United (Kirafiki, Kahama hakufungwa)
Simba SC 1-2 URA (Kirafiki, Taifa, alifungwa mbili)
Simba SC 0-1 Coastal (Kirafiki, Tanga alifungwa moja)
Simba SC 4-1 SC Villa (Simba Day, Taifa alifungwa moja)
Simba SC 2-2 Rhino (Ligi Kuu, alifungwa mbili)
Simba SC 1-0 JKT Oljoro (Ligi Kuu, hakufungwa)
Simba SC 2-0 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu, hakufungwa)
Simba SC 6-0 Mgambo JKT (Ligi Kuu, hakufungwa)

Mechi ya kwanza Dhaira kuidakia Simba SC ilikuwa ni dhidi ya Bandari Uwanja wa Amaan, Zanzibar katika Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu, ambako alifungwa bao moja, timu hiyo ikitoa sare ya 1-1.

Baada ya hapo, akaidakia Simba ikicheza dhidi ya U23 ya Oman, ambako alifungwa moja, timu hiyo ikifungwa 2-1 na akadaka dhidi ya timu ya Jeshi Oman na kufungwa mara mbili, timu hiyo ikilala 3-2. Bao lingine alifungwa Juma Kaseja, ambaye ametemwa msimu huu.

Akadaka tena katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Recreativo de Libolo ya Angola na kufungwa mabao manne, timu hiyo ikilala 4-0.

Akarudi Dar es Salaam na kudaka katika mchezo wa Ligi Kuu msimu uliopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga na kufungwa bao moja, timu hiyo ikishinda 2-1.

Akadaka tena katika Ligi Kuu dhidi ya Azam na kufungwa kafungwa mabao mawili, moja la penalti timu hizo zikitoka 2-1, huo ukiwa mchezo wake wa mwisho Simba SC msimu uliopita.

Akarejea kwenye mechi za kujiandaa na msimu huu, akadaka dhidi ya Kahama United mkoani Shinyanga na kwa mara ya kwanza tangu ajiunge na timu hiyo alifanikiwa kumaliza mechi bila kufungwa.

Akadaka tena dhidi ya URA ya kwao, Uganda katika mchezo wa kirafiki na kutunguliwa mara mbili timu hiyo ikilala 2-1 katika mchezo huo wa kirafiki, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Akaenda Tenga kwenye mchezo wa kirafiki na Coastal, akafungwa moja, Wekundu wa Msimbazi wakilala 1-0.

Akadaka tena dhidi ya SC Villa ya kwao, Uganda na kufungwa bao moja, timu hiyo ikishinda 4-1 kabla ya kufungwa mawili katika sare ya 2-2 na Rhino, hiyo ikiwa mara ya mwisho nyavu zake kutikiswa.

Sasa yuko madhubuti; Abbel Dhaira ameanza kuwa tishio Ligi Kuu ya Bara
Kisoka, Dhaira aliibukia Express mwaka 2006 ambako alicheza hadi 2008 akahamia URA, alikocheza hadi 2010 akahamia AS Vita ya DRC ambayo ilimuuza IBV mwaka 2012 alikodaka mechi 30 bila kufungwa bao hata moja, hadi anahamia Simba mwaka huu.

Amekuwa akiidakia timu ya taifa ya Uganda tangu mwaka 2009 na tangu 2011 amekuwa kipa namba moja wa timu hiyo, ingawa kwa sasa anakabiliwa na ushindani wa aliyekuwa kipa wa kwanza wa timu hiyo kabla yake, Dennis Onyango pamoja Muwonge Hassan anayeibukia vizuri.

Ndiyo basi tena; Juma Kaseja kulia alikuwa akizungumziwa kurejeshwa Simba SC wakati Abbel Dhaira hafanyi vizuri. Kushoto Amri Kiemba
Dhaira alidaka mechi moja tu na kuumia katika Kombe la Challenge mwaka jana na baada ya hapo, Muwonge akadaka hadi kuipa timu ubingwa. Muwonge tena akaipa Uganda tiketi ya CHAN- na sasa anajitengenezea mazingira mazuri The Cranes mbele ya Onyango na Dhaira.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC