Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAMBWE, KAZE SASA KUKIPIGA SIMBA, MOTO WAO UTAWAKA DHIDI YA OLJORO

Hatimaye wachezaji wapya wa Simba kutoka Burundi mshambuliaji Amisi Tambwe na beki Gilbert Kaze (Pihani) kutoka Burundi, jana walipata uhamisho wa kimataifa kwa ajili ya kuanza kuichezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, ilielezwa jijini Dar es Salaam jana.


Tambwe na Kaze juzi Jumamosi walishindwa kuitumikia timu yao hiyo kutokana na kukosa ITC na kusababisha mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, juzi asafiri kwenda Burundi kukamilisha usajili wa wachezaji hao.

Tambwe na Kaze waliwasili nchini wiki iliyopita na siku iliyofuata walielekea Kahama, Shinyanga kuungana na wachezaji wengine wa Simba ambao walikuwa wameweka kambi mkoani humo kujiandaa na msimu mpya wa ligi ulioanza Jumamosi.

Akizungumza na mtandao huu, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kuwa tayari wamekamilisha uhamisho wa wachezaji hao na keshokutwa Jumatano watashuka uwanjani kuitumikia timu hiyo kwa mara ya kwanza watakapoivaa JKT Oljoro kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

"Tumekamilisha mchana huu (jana mchana), Jumatano watacheza, tunashukuru tumewapata," alisema Mtawala.

Alieleza kwamba usajili huo umefanikishwa na safari ya mwenyekiti, Ismail Aden Rage, ambaye juzi alilazimika kusafiri hadi Burundi kwenda kukamilisha usajili huo kufuatia 'siasa' kuanza kuingia baada ya nchi hiyo kuona kwamba itawakosa wachezaji hao katika mechi za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) zitakazofanyika mapema mwakani.

Aliongeza kuwa suala la Betram Mwombeki na klabu yake ya zamani ya Pamba ya jijini Mwanza pia limefanyiwa kazi kwa kuwapa Sh. milioni mbili ili kubariki uhamisho huo.

Aliwataka mashabiki wa Simba kuwa na utulivu na matokeo mazuri yatapatikana katika timu yao.
Simba ilianza kwa sare ya magoli 2-2 dhidi ya Rhino Rangers ambayo imepanda daraja na kucheza Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu ilipoanzishwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC