Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAMBWE AANZA MCHECHETO LIGI KUU, ADAI NI NGUMU KULIKO KWAO BURUNDI

Baada ya kucheza kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mshambuliaji Amisi Tambwe (Pichani) wa Simba amesema ligi hiyo ni ngumu ukilinganisha na Ligi Kuu ya Burundi aliyotokea.


Tambwe, mfungaji bora michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) mwaka huu, ametua Simba akitokea Vital'O inayoshiriki Ligi Kuu ya Burundi. Akizungumza jana asubuhi kwenye hoteli ambayo Simba walikuwa wamefikia jijini hapa, Tambwe alisema alishindwa kuziona nyavu katika mechi yao ya juzi dhidi ya Oljoro kwa sababu alikumbana na vikwazo vingi uwanjani.

"Kwa kweli ligi ya Tanzania ni ngumu kuliko ya kwetu (Burundi). Timu zinakamia sana. Nilifanya kila mbinu ili nifunge lakini uwanja ulikuwa tatizo.

Haikuwa rahisi kukimbia huku ukimiliki mpira," alisema Tambwe. "Wapinzani wetu walikuwa wametukamia ndiyo maana ilibidi nicheze kwa tahadhari nikihofu kuvunjwa viungo. "Tunashukuru Mungu kwa kupata ushindi na mashabiki wetu watusamehe kwa kupoteza nafasi nyingi.

"Mechi ya jana karibu kila kitu kilikuwa kigeni kwangu - uwanja, mfumo wa Simba na hata wachezaji wa timu yetu.

Ukiwaondoa Chollo, Kiemba na Kaze, wengine wapya ni kwangu. Nahitaji muda kuwasoma."
Baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Kagame ambayo mwaka huu ilifanyika Sudan, Tambwe na Mrundi mwenzake beki Gilbert Kaze walisaini mikataba ya miaka miwili kuitumikia Simba.

Wawili hao, ambao pia ni wachezaji tegemeo katika timu ya taifa ya Burundi, walitoa mchango mkubwa katika klabu ya Vital'O waliyoipa ubingwa wa Kombe la Kagame Julai.

Kaze na Tambwe pia wamesaidia kuivusha Burundi kushiriki Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), nafasi ambazo wawili hao tayari wamejivua ushiriki baada ya kusaini kuichezea Simba ambayo iko nje ya nchi yao.

Hadi anatua Simba wiki iliyopita, Tambwe alikuwa anaongoza safu ya wafungaji wa ligi kuu ya Burundi akiifungia Vital'O magoli 21 katika mechi 18 msimu huu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...