Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAJIRI WA CHELSEA AKATISHA UFADHILI WAKE KWENYE SOKA

Mfanyabiashara tajiri na mmiliki wa klabu ya Chelsea, Roman Abramovich (Pichani) amesema amesitisha ufadhili wake wa soka nchini Urussi.


Msemaji wa kampuni ya uwekezaji ya Millhouse inayomilikiwa na Abramovich, amesema, chuo cha mafunzo ya soka nchini Urusi kilichokuwa kikifadhiliwa na mfanyabiashara huyo kimeafikia malengo yake.

Mtandao wa Forbes umechapisha habari kuwa tangu mwaka wa 2010, Abramovich amekuwa akipunguza ufadhili wake kwa shughuli za kuimarisha soka nchini Urusi.

Hata hivyo hakuna mzozo wowote uliosababisha uamuzi huo.
Ripoti zinasema kampuni ya NFA ilifadhili ujenzi wa viwanja mia moja thelathini nchini Urusi na kutumia zaidi ya dola milioni mia mbili.
Kampuni hiyo iliyoundwa mwaka wa 2004, pia iligharamia mafunzo ya makocha nchini Urusi.

Abramovich alianza kufadhili soka nchini Urussi muda mfupi baada ya kununua klabu ya Chelsea inayoshiriki ligi kuu ya Premier ya Uingereza.

Tangu mwaka wa 2005 hadi mwaka wa 2010 Abramovich alisaidi kufadhili timu ya taifa ya soka ya Urussi, ikiwa ni pamoja na mshahara wa dola milioni saba kwa kocha wake Guss Hiddink raia wa Uholanzi.
Dick Advocaat aliteuliwa kuwa kocha wa Urusi mwaka wa 2010 kuchukua mahala pa Hiddink.

Lakini mwaka wa 2010 Urussi ilishindwa kufuzu kwa fainali ya kombe la dunia iliyoandaliwa nchini Afrika Kusini.

Jarida la Forbes limechapisha ripoti kuwa Abramovich anashikilia nafasi ya kumi na tatu miongoni mwa watu tajiri zaidi nchini Urusi na inakadiriwa kuwa ana mali inayokisiwa kuwa zaidi ya dola bilioni kumi nukta mbili

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...