Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STEPHEN KESHI HATARINI KUFUNGIWA NA FIFA

Shirikisho la mchezo wa soka duniani FIFA, limethibitisha kuwa limepokea malalamishi kutoka kwa shirikisho la mchezo wa soka nchini Malawi FAM, kuhusiana na matamshi yaliyotolewa na kocha wa Nigeria, Stephen Keshi (Pichani).

Hata hivyo shirikisho hilo la FIFA limesema kuwa kwa sasa haliwezi kusema lolote kuhusu suala hilo, hadi uchunguzi utakapo kamilika.
FAM limedai kuwa Keshi alitoa matamshi ya ubaguzi dhidi ya kocha wake Tom Sainfiet raia wa Ubelgiji.
Katibu mkuu wa FAM, Suzgo Nyirenda ameiambia BBC, kuwa matamshi hayo ya ubaguzi hayafai kuwepo katika michezo katika dunia ya sasa.
''Tunahisi na shambulio dhidi ya kocha wetu na tutamtetea kwa hali na mali, bila kuzingatia uraia wake na rangi ya ngozi yake'' Alisema Nyirenda.
''Tumetuma ushahidi wa yale Keshi aliyoyasema na tunatarajia kuwa FIFA itachukua hatua kali dhidi ya kocha huyo wa Nigeria Stephen Keshi'' aliongeza Nyirenda.
Kesi hiyo inahusiana na matamshi ambayo Keshi aliyatoa kufuatua wito wa Malawi wa kuhamisha mechi yao ya kufuzu kwa kombe la dunia mwaka wa 2014, kutoka mji wa Calabar kutokana na sababu za kiusalama.
Katika mahojiano na runinga moja ya Uingereza, Keshi alisema ''Nafikiria kuwa kocha huyo wa Malawi ni wazimu''.
''Ikiwa anataka kuongea na FIFA, basi ni lazima arejea kwao nchini Ubelgiji. Yeye sio mtu wa Afrika, ni mzungu mweupe, ni lazima arudi kwao Ubelgiji'' Alisema Keshi katika mahojiano hayo.
Maafisa wakuu wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria pamoja na kocha huyo hawajasema lolote kuhusiana na madai hayo ya kocha wa Malawi Saintfiet na FAM.
Mechi hiyo kati ya Malawi na Nigeria mjini Calabar itaamua nani atafuzu kwa raundi ya mwisho ya mechi ya kufuzu kwa fainali hiyo barani Afrika.
Mabingwa hao wa Afrika wanahitaji kutoka sare ya aina yoyote ili kufuzu ili hali Malawi inahitaji ushindi ili isonge mbele.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC