Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YAUMBULIWA NA RHINO, PENGO LA KASEJA LAONEKANA

Simba jana ilianza kwa lawama na majanga msimu mpya wa ligi kuu ya Bara baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na timu ya Rhino Rangers iliyopanda daraja kwa mara ya kwanza na ambayo Wekundu wa Msimbazi walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kuifunga.

Mara baada ya pambano hilo kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi hapa, kocha wa Simba Abdallah Kibadeni alisema matokeo hayo yamesababishwa na Abel Dhaira kufungwa magoli ya kizembe langoni mwa timu hiyo ya Msimbazi.
Saddy Kipanga ndiye aliyeifungia Rhino bao la kusawazisha dakika 25 kabla ya filimbi ya mwisho kwa shuti kali la mpira wa adhabu ndogo kutoka mita 20, ambalo lilimpita ubavuni Dhaira katika lango la Simba.
Adhabu ndogo hiyo ilikuwa imetolewa na muamuzi Amon Paul baada ya Issa Rashid 'Baba Ubaya' kumkwatua mchezaji wa zamani wa Simba Nurdin Bakari nje kidogo ya eneo la hatari.
Bao hilo liliamsha shangwe za watazamaji takribani 20,000 waliohudhuria mechi ya kwanza ya ligi kuu ya Bara mjini Tabora katika miaka 14, tangu Milambo iliposhuka daraja 1999.
Jonas Mkude aliifungia Simba bao la kwanza katika dakika ya 12 kwa kichwa kutokana na mpira wa kona iliyopigwa na 'Baba Ubaya' na kuweka matumaini ya kufanya kile ambacho wachambuzi wa soka walitaraji.
Lakini ndoto hiyo ilianza kuingia dosari dakika nane kabla ya mapumziko, wakati Iman Noel alipoifungia Rhino bao la kwanza kwa mpira wa adhabu ndogo kutoka nje kidogo ya eneo la hatari.
Adhabu hiyo ambayo ilimshinda Dhaira kwa staili ile ile ya goli la pili la wenyeji, ilitolewa baada ya beki Mirani Athumani wa Simba kumrukia mgongoni Victor Hangaya.
Mkude aliifungia Simba bao la pili katika dakika ya 41 baada ya muamuzi Paul kuamuru tuta hilo kutokana na Stanslaus Mwakitosi kumuangusha Amri Kiemba ndani ya 18.
Timu zilikuwa:
RHINO: Abdulkarim Mtumwa, Ally Ahmed, Hussein Abdallah, Julius Masunga, Laban Kambole, Stanslaus Mwakitosi, Daniel Manyenya (abbas Mohammed dk.66), Iman Noel, Victor Hangaya, Nurdin Bakari, Sady Kipanga.
SIMBA: Abel Dharia, Nassoro Masoud, Issa Rashid, Miraji Adam, Joseph Owino, Jonas Mkude, Ramadhani Chombo (Ramadhani Singano dk.62), Ndemla Said, Amri Kiemba, Betram Mwombeki (William Lucian dk.36), Haruna Chanongo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...