Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KAMILI GADO KUIVAA JKT OLJORO, TAMBWE, KAZE YAWAPA JEURI



Baada ya uongozi wa Simba kufanikiwa kupata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) za nyota wao wa kigeni Warundi, Amisi Tambwe na Gilbert Kaze, meneja wa timu hiyo, Mosses Basena (Pichani) amesema kikosi chao sasa ni ‘moto wa kuotea mbali’.


Akizungumza jana akiwa Arusha, Basena alisema anaamini nyota hao watakisaidia kikosi cha ‘Wanamsimbazi’ kilicholazimishwa sare ya 2-2 dhidi ya ‘maafande’ wa Rhino Rangers katika mechi yao ya ufunguzi wa msimu huu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora Jumamosi.

“Tunashukuru Mungu tulifika salama Arusha jana (juzi) saa mbili usiku. Tumefarijika kupata ITC za wachezaji wetu (Tambwe na Kaze) ambao walizuiwa kucheza Tabora,” alisema Basena.

“Tambwe na Kaze ni wachezaji wazuri. Naamini wataiimarisha timu yetu. Kikosi chetu sasa kimekuwa moto na hatuna wasiwasi wa kufanya vibaya katika mechi zijazo,” aliongeza Mganda huyo.

Mshambuliaji Tambwe na beki wa kati Kaze, ambao walilazimika kuwa watazamaji katika mechi ya Jumamosi baada ya Shirikisho la Soka (TFF) kuwazuia kucheza kutokana na kutokuwa na ITC, wameingia mikataba ya miaka miwili na Simba wakitokea klabu ya Vital’O ya Burundi, waliyoipa ubingwa wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) mwaka huu.

Katika mashindano hayo ya Kombe la Kagame, ambao mwaka huu timu za Simba, Yanga na Super Falcon za Tanzania hazikushiriki kwa hofu ya usalama wa nchini Sudan, ambako mashindano hayo yalifanyika, Tambwe aliibuka mfungaji bora.

Kabla ya kutua Simba, Tambwe pia aliifungia Vita’O magoli 21 katika mechi 18 za msimu huu wa Ligi Kuu ya Burundi, na ndiye anaongoza kwa magoli katika ligi hiyo.

Aidha, Basena ambaye aliwahi kuwa kocha wa Simba, alisema kikosi chao kinaendelea vyema na maandalizi ya mechi yao ya pili ya ligi hiyo dhidi ya Oljoro JKT itakayopigwa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kesho.

“Mechi ya Jumatano (kesho) itakuwa ngumu ukizingatia wapinzani wetu wako nyumbani na walipoteza mechi yao ya kwanza Jumamosi,” alisema.

Oljoro JKT ilianza vibaya msimu huu baada ya kulala 2-0 nyumbani dhidi ya mabingwa wa mwaka 1988 wa Tanzania Bara, Coastal Union katika mechi yao ya ufunguzi wa msimu huu kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Jumamosi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC