Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ROMA MKATOLIKI AFANYA MAKAMUZI YA HATARI DAR

Msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Roma Mkatoliki na bendi ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twnaga Pepeta' walikonga nyoyo za mashabiki tele waliojitokeza katika bonanza maalum lililoandaliwa kwa udhamini wa kinywaji cha Vita Malt kwenye viwanja vya Posta, Kijitonayama jijini Dar es Salaam juzi.


Roma Mkatoliki alipagawisha watu zaidi kutokana na vibao vyake vikali kama 'Tanzania' na 'Mathematics', huku mashabiki wakimshangilia zaidi kutokana na namna alivyokuwa akighani mashairi yake kwa hisia kali.

Kiongozi wa Twanga Pepeta, Luiza Mbutu, alishirikiana na wenzake katika kunogesha zaidi bonanza hilo kutokana na uimbaji wao na kucheza kwa kujituma kuanzia mwanzo hadi mwisho, hivyo kuwa kivutio kwa kila aliyehudhuria.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa bonanza hilo, Meneja wa Vinywaji visivyo na Vileo katika Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Consolata Adam, alisema kuwa  waliamua kuandaa tamasha hilo kwa nia ya kuwakutanisha pamoja wafanya mazoezi wote kutoka katika vituo maalumu (gym).

“Tuliamua kuandaa bonanza linalowakutanisha wanamichezo mbalimbali, hasa wafanya mazoezi ili wajumuike pamoja katika kufanya mazoezi," alisema, akiongeza kuwa wanamichezo kutoka katika vituo 10 vya gym walishiriki bonanza hilo, wakiongozwa na wakufunzi kumi ambao waliongozwa na mkufunzi wa kimataifa Shadrack Opulukwa.

Alizitaja gym zilizoshiriki kuwa ni Better Life, Genessis ya Kijitonyama, Segerea Gym, Rio Gym, Genessis ya Kimara, Azula ya Mikocheni na Serena Gym.

Kivutio kikubwa katika bonanza hilo ilikuwa ni ushindani kutokana kwa baa za Fyatanga ya Tegeta na Kisuma ya Temeke, ambazo zilionyeshana umwamba katika kuandaa nyama bomba.

Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa TBL, Edith Mushi, alisema wanashukuru kwa kiasi kikubwa kufanikiwa kwa bonanza hilo kwani wamesaidia pia kujenga afya za Watanzania.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC