Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NI CHEKA AU MMAREKANI KUIBUKA MBABE LEO!

Pambano la ngumi la kimataifa kati ya bondia Francis Cheka wa Morogoro na Phil 'The Drill' Williams (Pichani) wa jimbo la Minneapolis, Minnesota nchini Marekani la kuwania mkanda unaotambuliwa na Shirikisho la Ngumi Duniani (WBU) linatarajiwa kufanyika leo kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.


Akizungumza jana kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo), Rais wa WBU, Golden Howard, alisema kuwa maandalizi ya pambano hilo yamekamilika na mabondia wameshaelezwa taratibu za kuwania mkanda huo.

Howard alisema kuwa pambano hilo litasimamiwa na majaji watatu na kati ya hao wawili ni Watanzania na mmoja ametoka Afrika Kusini ambaye tayari aliwasili nchini tangu juzi.

Rais huyo aliwataka mabondia hao kuonyesha mchezo mzuri katika pambano hilo la hadhi ya juu linalotarajiwa kuvutia wadau mbalimbali wa mchezo huo wa ndani na nje ya nchi.

Cheka ambaye ana rekodi nzuri nchini baada ya kupima uzito alitamba kufanya vizuri katika pambano hilo huku akieleza kuwa anafahamu anakutana na mpinzani mwenye uzoefu wa kimataifa.

"Nimejiandaa vyema na naamini sitawaangusha Watanzania wenzangu, niko fiti kila idara," alisema Cheka.

Williams naye alitamba kwamba amekuja Tanzania kusaka ushindi na amejipanga kumpiga Cheka kwa KO.
"Nitampiga kwa KO mpinzani wangu, hatachukua muda," alisema kwa kifupi Williams ambaye muda wote alikuwa akinywa maji pamoja na matunda ya apple.

Wakati huo huo, Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa  Nchini (TPBC), Yasin Abdallah, alisema kuwa mpinzani wa Alphonce Mchumiatumbo kutoka Marekani, DeAndre 'Showtime' McCole hadi jana alikuwa hajawasili nchini kutokana na kutoka tiketi na hivyo sasa atapigana na bondia mwingine wa hapa nchini.

Yasin aliwataka mabondia wote kuwahi kufika ukumbini kama taratibu za mchezo huo zinavyoeleza kimataifa ili wapate muda wa kupumzika wakiwa ukumbini hapo.

"Tunatarajia kuwa na wageni wakubwa, huenda Rais (Jakaya) Kikwete na Waziri wa Michezo (Fenella Mukangara) watakuwapo, ule ushabiki wa kihuni usiwepo," aliongeza.

Mratibu wa pambano hilo, Jay Msangi, alisema kuwa maandalizi yamekamilika kama walivyopanga na wanaamini pambano hilo litaweka historia nyingine ya ngumi nchini kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Alitaja mapambano mengine ya utangulizi yatakayokuwapo leo kuwa ni la raundi 12 kuwania la kuwania ubingwa wa mkanda wa Afrika uzito wa juu wa kati (Super Middle) ambapo Mada Maugo (15-9, KO 11) aliye namba tatu kwa ubora nchini atakapopambana na Thomas Mashali (8-1, KO 5) wote wa hapa nchini huku Cosmas Cheka (8-3) atapigana na Alan Kamote (20-6, KO 12) katika pambano la raundi sita.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC