Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MWAISABULA APINGA PENALTI YA COASTAL

Mkwaju wa penalti wa dakika za mwisho waliopewa Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga na Mwamuzi Martin Saanya, umepokelewa kwa hisia tofauti na wadau wa soka nchini.


Kocha mzoefu, Kenned Mwaisabula "Mzazi" (Pichani) aliuambia mtandao huu jana kuwa mwamuzi hakustahili kutoa pigo la penalti kwa Coastal kutokana na umbali aliokuwepo wakati tukio likitokea.

“Saanya (Martin) hakustahili kutoa penalti ile kwa Coastal. Nasema hivi kutokana na umbali aliokuwepo wakati tukio lile linafanyika. Nadhani alikuwa umbali wa mita 15.”

“Kwa maana hiyo mwamuzi wa pembeni ndiye aliyekuwa karibu na tukio lile, lakini hakuonyesha alama yoyote kuashirikia kuna tukio limefanyika.”

Hata hivyo, kocha wa Yanga, Ernie Brandts alikiri kuwa penalti hiyo ilikuwa halali na hana sababu ya kuipinga, lakini ameshutumu kadi nyekundu ya  Simon Msuva.

Wakati huohuo, Klabu za Yanga na Coastal Union zimejiweka kwenye hatari ya kulimwa faini ya Sh500,000 kila moja baada ya wachezaji wake kupata kadi zaidi ya tano katika mchezo baina ya timu hizo.

Kwa mujibu wa kanuni ya 27 ya udhibiti wa wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania kifungu (d), timu ambayo wachezaji wake wataonyeshwa kadi zaidi ya tano katika mchezo mmoja itatozwa faini ya Sh500,000.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...