Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAKALA: 'MATRAFIKI FEKI' TUNAO WENGI KWENYE MICHEZO

Kwa sasa kila kitu kinaendeshwa kiujanjaujanja, kama imetokea mtu kujipenyeza na kujipa ajira ya uaskari wa barabarani (traffic) kwa vitu vingine ni rahisi tu, tena  kichekesho eti alianza kazi hiyo mjini Singida.


Alijipa uhamhisho yeye mwenyewe pasipo mwajili wake mkuu, 'trafiki feki' huyo alihamia jijini Dar es salaam jiji la wajanja unaweza kuliita hivyo.

Akiwa hapa jijini trafiki huyo wa kuchonga alijitupa eneo la Kinyerezi na kuendelea  kuyapiga mabao magari yanayokiuka sheria yaani alizijua sheria zote na kuzigundua gari zinazocheza rafu barabarani.

Kwanza nampongeza kwa weledi wake huo wa kuyatambua magari yanayocheza rafu, kisha namponda kwa maamuzi yake ya kujifanya trafiki, Licha ya kujifanya trafiki wapo waliojifanya Wanajeshi ama usalama wa taifa.
Nini usalama wa usalama, Kuna watu wanajifanya mawaziri na kuwapigia watu simu na kutaka fedha, hivi karibuni kuna jamaa alijifanya yeye ndio waziri wa mambo ya ndani.

Akataka kuvuta mpunga lakini dili ikakataa, Aliyempiga kirungu ni mtoto wa mjini alishituka labda kwa sababu ya trafiki feki ambaye amejanjarusha wengi.

Jiji la Dar es Salaam lenye wajanja wengi lakini bado limeshindwa kuwabaini matapeli wa namna hii wanaojifanya trafiki feki au usalama wa taifa.


Jamaa huyo huenda aliyemchoma kwa jeshi la polisi ni mtu anayemfahamu
Kama mtu aliweza kujifanya trafiki tena kuanzia Singida hadi Dar es Salaam inaonyesha wapo watu wengi waliojichomeka kwenye idara nyeti nchini bila ya kugundulika.

Trafiki feki amekusanya zaidi ya mamilioni mpaka alipodakwa, mambo hayaendi vizuri, uchumi wetu unachezewa na wajanja wachache ambao wanatuyumbisha, licha ya tafiti mbalimbali kuonyesha kwamba uchumi wa Tanzania unakuwa kwa kasi bado tunapata wasiwasi juu ya ukuaji wa uchumi wetu.

Uingizaji wa madawa ya kulevya umezidi kwa kasi tena mno kiasi kwamba waziri wa uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe kuingilia kwa nguvu zote,
Mwakyembe ameamua kupambana na watu wanaoingiza dawa za kulevya hapa nchini ina maana ulinzi wote uliokuwepo pale uwanja wa ndege Mwl Julius Nyerere lakini wajanja wanapitisha 'Bwimbwi'kiurahisi.

Hata mbwa wanotumika kugundua uharifu nao ‘feki’ kwa usalama wa taifa usiseme huko ndio wamejificha maofisa feki wanaodhulumu jasho la Watanzania.

Sitaki kuelezea kwa undani nisijeng’olewa kucha bure au kumwagiwa ‘tindikali’ matrafiki feki tunao wengi kwenye medani ya michezo hasa soka.

Huku kuna idadi kudwa kwa sababu soka inalipa wakishaingia tu huja na nguvu kubwa wakishafanikiwa hutokomea ghafla kama soka lipo kwenye damu kamwe huwezi kuliacha.

Wako wapi akina Jack Pemba, Alex Kajumulo na wengine wenye nguvu kama hao, walikuja na miradi mikubwa ya kuwekeza kwenye mchezo wa soka walishiriki kusaini mikataba minono lakini wakaingia mitini.

Sishangai ninapoona ahadi mabalimbali zinazotolewa na viongozi wetu wa soka hasa Simba na Yanga kukwama ni kutokana na 'trafiki feki' kuna uwezekano wengine kujulikana kupitia michezo.

Simba na Yanga zinaongozwa na 'matrafiki feki' ambao badala ya vilabu viwategemee wao, ni tofauti kidogo wao ndio wanazitegemea klabu hiko ni kichekesho kikubwa sana.

Klabu hizo zote kwa pamoja zilianzishwa na mababu zetu waliopigana kwa jasho lao miaka 77 iliyopita mababu hao waliweza kujenga misingi imara ambayo imeachwa kama urithi, majengo ni moja kati ya urithi wao ambayo yanatumika hadi sasa kama vitega uchumi.

Lakini ‘matrafiki feki’ waliopo miaka hii ya hivi karibuni wameshindwa kuziletea maendeleo zaidi, wamegeuka mahiri kwa mazungumzo Kwa kifupi Simba na Yanga hazina cha kujivunia isipokuwa kugombea wachezaji ndicho wanachoweza, utasikia mwaka huu wanamgombea Mbuyu Twite au Kelvin Yondani, mwaka mwingine Mrisho Ngassa.

Ipo siku sasa watafikia kugombea makocha au viongozi kila mmoja akidai huyo wa kwake, kwenye shirikisho letu la soka nchini TFF nako limevamiwa na ‘matrafiki feki’ sioni kama kuna mabadiliko ya kweli ni propaganda tu.
 Kupaka rangi ndiyo desturi yao ya kila siku lakini maendeleo hakuna maana ninavyoijua Tanzania! ya miaka iliyopita si hii ya sasa, Michezo yote imedorola hapa nchini wanaopewa dhamana ya kuongoza si wanamichezo wenye uchungu wa kweli, wengi wanajikita kwenye uongozi kwa malengo yao binafsi.

Ndiyo maana michezo mingine imekosa mashabiki kutokana na aina hii ya viongozi kama iliwezekana kumnasa trafiki feki aliyekuwa pale Kinyerezi basi itawezekana kuwabaini trafiki wengine waliojazana Kwenye idara nyeti ikiwemo michezo.

Wanachama wa Simba na Yanga kama mtashirikiana kwa dhati inawezekana kuwanasa wale matrafiki feki waliojipenyeza ndani ya vilabu vyenu ambao wanazitumia timu hizo kama kitega uchumi chao.

Ama sivyo umasikini kwa vilabu hivyo hautakwisha na itakuwa tatizo la timu hizo kuwa na viwanja vyake huku mkirushwa roho na habari za usajili kila kipindi chake kinaponza.

Usajili wenyewe wa kunyang’anyana wachezaji badala ya kutegemea matunda yanayotokana na uwekezaji mzuri wa vikosi vya pili vinavyotokana na akademia, kweli viongozi wa timu na shirikisho wengi wao ni matrafiki feki na ikibidi wachunguzwe ili waondolewe ama sivyo mambo hayawezi kusonga mbele.

Kila siku tunalia kuwa Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu hata rais wa awamu ya pili Alhaj Ally Hassan Mwinyi aliwahi kutamka kauli hiyo, Tumechoka sasa kuburuzwa, tuonane wiki ijayo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC