Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HENRY JOSEPH SHINDIKA KUTAMBULISHWA SIMBA JUMAPILI

KOCHA Mkuu nwa Simba SC, Alhaj Abdallah ‘King Kibaden’ amelainika kwa Mwenyekiti wa klabu yake, Alhaj mwenzake, Ismail Aden Rage na kukubali timu hiyo icheze mchezo wa kirafiki Jumapili Dar es Salaam na Mafunzo ya Zanzibar.


Mchezo huo ni maalum kuwatambulisha wachezaji wapya wa Simba SC, Warundi, beki Kaze Gilbert na mshambuliaji Tambwe Amisi baada ya kupatiwa Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC).

Mchezo huo utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, pia utatumika kumtambulisha kiungo Henry Joseph (Pichani) aliyesajiliwa tena Simba SC akitokea Kongsvinger ya Norway ambako alikwenda mwaka 2009 akitokea kwa Wekundu hao wa Msimbazi baada ya kupiga kazi tangu mwaka 2005

Awali, Kibadeni alikataa timu kucheza mechi hiyo na akasema icheze Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya mchezo wa jana wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania na JKT Oljoro, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, ambao Simba ilishinda 1-0, bao pekee la Haroun Athumani Chanongo dakika ya 34.

Lakini baada ya ‘wakubwa’ hao kuzungumza wameafikiana na sasa Wekundu wa Msimbazi watakipiga na Mafunzo Jumapili Taifa na Mwandaaji wa mchezo huo, George Wakuganda amesema maandalizi yanaendelea vizuri na wana Simba watarajie burudani muruwa siku hiyo.

Mwenyekiti huyo wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage alilazimika kwenda Burundi kufuata ITC za wachezaji hao mwishoni mwa wiki baada ya kuona zinachelewa kufika nchini, hivyo kuwachelewesha pia kuanza kazi.

Rage aliondoka Dar es Salaam Jumamosi usiku na ndani ya saa 24 alifanikisha suala hilo na hiyo ilikuwa mara ya pili kwa Rage, ambaye ana uzoefu wa kuongoza soka kwa zaidi ya miongo mitatu, kuingilia kati suala la uhamisho wa wachezaji wa kimataifa na kufanikisha baada ya miaka miwili iliyopita, kusafiri hadi Jamhuri ya Afrika ya Kati kushughulikia ITC ya mchezaji Gervais Kago ambao nao ulikuwa na matatizo.

Baada ya kupata ITC hizo, Kaze na Tambwe walianza kazi rasmi jana Simba SC katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya JKT OIjoro ya Arusha jana mjini Arusha na kuchangia ushindi wa kwanza katika Ligi Kuu. Simba tayari imewakatia wachezaji hao vibali vya kufanya kazi hapa nchini.

Wachezaji wengine wa kigeni wa Simba, Waganda Joseph Owino na Abel Dhaira, wamecheza mechi zote mbili za awali za Ligi Kuu, kutokana na kukamilishiwa taratibu zote za uhamisho na kuwa na vibali vya kufanya kazi hapa nchini.

Kaze na Tambwe waliosajiliwa kutoka mabingwa wapya wa Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, Vital’O ya kwao, Jumamosi walikuwapo Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora kuishuhudia timu yao ikilazimishwa sare ya 2-2 na Rhino katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC