Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GAZETI LA NIPASHE KUDHAMINI MISS TANZANIA



Gazetila NIPASHE jana lilitangaza kuwa limedhamini shindano la urembo nchini la Miss Tanzania 2013.

Simon Marwa (Pichani), Meneja wa Masoko wa Kampuni ya The Guardian Limited inayochapisha gazeti la NIPASHE, alisema NIPASHE imejitokeza kudhamini mashindano hayo kwa nia ya kusaidia kukuza sanaa ya urembo nchini.

"NIPASHE ikiwa ni moja kati ya magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya The Guardian Limited, kwa kutambua umuhimu wa mashindano haya, imeamua kuwa moja kati ya wadhamini wa Miss Tanzania 2013 kama njia ya kukuza mashindano haya," alisema Marwa. 

Aliongeza kwamba kwa kupitia udhamini huo, warembo watakaoshiriki watapata fursa ya kutambulika nchi nzima.

"Vile vile udhamini huu unalenga kuwapatia wapenzi wa urembo na mitindo burudani na matukio kemkem ambayo yatajiri katika mchakato mzima wakumpata Miss Tanzania 2013 kupitia gazeti la NIPASHE," aliongeza.

NIPASHE imekuwa mstari wa mbele kwenye kudhamini matukio tofauti nchini kama ilivyofanya katika mashindano ya Miss Tabata 2013, na Marwa alisisitiza kwamba huo ni mwanzo tu.

"Tutaendelea na mwendo huu wa kudhamini hata matukio mengine ambayo yana lengo la kuleta matokeo chanya kwenye jamii yetu," alisema.

Aidha, warembo washiriki wa Miss Tanzania 2013, kwa nyakati tofauti walimwaga tambo kuelekea kwenye fainali za mashindano hayo wakati walipokutana na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Giraffe iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam jana.

Wengi wao walionekana kujiamini zaidi na kudai wana uhakika mkubwa wa kushinda taji hilo, ambalo kwa sasa linashikiliwa na Brigette Alfred.

“Kwangu nataka kufanya kweli zaidi, kwani najua wapi naweza kuwashinda wenzangu hawa,” alisema mrembo Elizabeth Pert anayetoka mkoa wa Pwani.

Janet Awet wa Lindi naye alijisifu akisema ana sifa zote za kutwaa taji, hivyo wenzake wajiandae kuwa wasindikizaji katika shindano hilo.

Lucy Charles wa Mwanza na Esha Rashid kutoka Mara nao walitoa tambo zao, huku Severina Lwinga na Mariam Manyanga (Kanda ya Vyuo), wakitamba kwamba wao ndiyo wana uhakika wa mmojawapo kuondoka na taji.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino, Hashim Lundenga ambao ndiyo waandaaji wa Redd's Miss Tanzania alisema, kwa sasa kila kitu kimekamilika na anaamini warembo hao wote wana sifa zinazostahili.
“Wasichana wote waliopo hapa wana sifa za kutosha, naamini kwa dhati kabisa Redd's Miss Tanzania kwa mwaka huu atakuwa na sifa zote zinazotakiwa.”

Meneja wa Redd’s, Victoria Kimaro naye alisema, kama wadhamini wapo tayari kuhakikisha shindano hilo linafanikiwa kwa kiasi kikubwa zaidi na kumtoa mrembo bora.

“Tunaamini kabisa kama Redd’s shindano hili litatoa mrembo bora zaidi kuliko kipindi chote kwani ukiwatazama unaona wana sifa zote,” alisema.

Warembo wanaoshiriki na kanda wanazotoka zikiwa kwenye mabano ni Happiness Watimanywa (Dodoma), Sabrina Juma (Tabora), Nice-Jack Herman (Singida), Anastazia Donald (Tabora), Linah Allan (Rukwa), Jacqueliene Luvansa (Mbeya), Neema Mality (Iringa), Diana Laizer, Sabra Islam (Moro), Janet Awet (Lindi) na Elizabeth Pert (Pwani).

Wengine ni Lucy Charles (Mwanza), Esha Rashid (Mara), Salsha Isdory (Geita), Severina Lwinga, Mariam Manyanga (Kanda ya Vyuo), Lucy James (Chuo Kikuu Huria), Svetlana Nyameyo (Kurasini), Narieth James (Chang’ombe), Latifa Mohamed (Kigamboni).

Wapo pia Lucy Tomeka (Dar Indian Ocean), Prisca Clement (Sinza), Philios George (Ubungo), Sarah Martin, Dorice Mollel (Tabata), Alice Isaac na Carol Bayo (Dar City Centre).

Chanzo cha habari                                                    NIPASHE

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC