Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHEKA AENDELEZA UMWAMBA WAKE, AMCHAKAZA MMAREKANI NA KUTWAA MKANDA WA DUNIA

BONDIA Mtanzania, Francis ‘SMG’ Cheka (Pichani akimdunda ngumu mpinzani wake) jana usiku ametawazwa kuwa bingwa mpya wa dunia wa WBF, katika uzito wa Super Middle baada ya kumshinda Mmarekani, Phil Williams kwa pointi katika pambano la Raundi 12, lililofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.


Jaji wa kwanza Eddie Marshall kutoka Afrika Kusini alitoa pointi 116 kwa 115, jaji wa pili Fidel Hayness alitoa pointi 119 kwa 118 na jaji wa tatu, John Chagu alitoa pointi 117 kwa 116 (wote wa Tanzania), wakimpa ushindi Cheka.

Kwa ushindi huo, Cheka amefuata nyayo za bondia mwingine Mtanzania, Rodgers ‘Tiger’ Mtagwa ambaye aliwapiga Wamarekani kadhaa kwao, ambako anaishi tangu 1998.

Bondia Francis Cheka wa Tanzania akimtupia konde Mmarekani, Phil Williams katika pambano la Raundi 12 kuwania ubingwa wa dunia uzito wa Super Middle usiku huu ukumbi wa Diamond Jubilee kuwania taji la WBF. Cheka ameshinda kwa pointi.

Miongoni mwa mabondia Wamarekani ambao Mtagwa, mtoto wa Keko Mwanga, Temeke, Dar es Salaam amewahi kuwapiga ni Garvin Crout kwa Knockout (KO) Raundi ya kwanza pambano la Raundi nane, kwenye ukumbi wa Blue Horizon, Philadelphia, Pennsylvania, Marekani pambano lililochezeshwa na refa James Condon Septemba 12, mwaka 2000 na mwingine Donovan Carey kwa KO pia Raundi ya Pili Juni 15, 2001 ukumbi huo huo.

Katika pambano hilo lililochezeshwa na refa kutoka Afrika Kusini, Drake Ribbinck, mabondia hao walianza kwa kusomana Raundi ya kwanza wakitupiana makonde ya tahadhari na katika Raundi ya pili, kila mmoja alitaka kuhakikisha kile alichogundua kwa mpinzani wake kabla ya kazi kuanza Raundi ya Tatu.
Cheka aling’ara katika Raundi ya Tatu na ya nne na Mmarekani akaibuka Raundi ya Tano na kuanza kuonyesha upinzani. Raundi ya Sita Mmarekani aliongeza kasi ya urushaji makonde na Raundi ya saba na ya nane walipigana sawa, ingawa Williams alianguka kwa kuteleza na kuinuka kuendelea na pambano.

Raundi ya 10 mabondia hao waliendelea kutupiana makonde kwa zamu, lakini Raundi ya 11 na 12 pamoja na Williams kusimama imara kutafuta ushindi wa Knockout (KO), lakini SMG alikuwa makini katika kukwepa na kurusha ngumi za kudonoa kichwani kwa mpinzani wake.

Na kwa sababu hiyo haikushangaza baada ya pambano, bondia mwenye maskani yake Morogoro kutangazwa bingwa mpya wa WBF.

Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara aliyekuwa mgeni rasmi alijaribu kwa tabu tabu kumvisha taji Cheka kutokana ulingo kuvamiwa na mashabiki waliopagawa na ushindi wa bondia huyo.

Katika mapambano ya utangulizi, Thomas Mashali alimshinda kwa pointi Mada Maugo, wakati Alphonce Mchumia Tumbo alimshinda kwa Technincal Knockout (TKO), baada ya wasaidizi wake kurusha taulo Raundi ya tano katika pambano la Raundi sita.

Hata hivyo, dosari  iliyojitokeza katika usiku huo ni mabondia kugoma kupanda ulingoni hadi kwanza walipwe fedha zao na ilianzia kwa Mchumia Tumbo, ikafuatia kwa Maugo na Mashali na baadaye Cheka.

Bingwa wa zamani wa dunia, bondia wa Afrika Kusini, Francois Botha alilaani hali hiyo na kusema mabondia wanapanda ulingoni kwa ajili ya fedha, hivyo kutokokuwa na uhakika wa malipo yao si sawa.

Alipoulizwa kuhusu malipo yake, Botha aliyewahi kupigwa kwa mbinde na bingwa wa zamani wa dunia, Mmarekani, Mike Tyson alisema yeye amekuja kwa mradi maalum wa kampeni kuzuia Malaria na hana anachodai kwa waandaaji wa pambano hilo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC