Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AKINA BALOTELLI WAFUZU HATUA YA MAKUNDI ULAYA

Wachezaji wa AC Milan
AC Milan ya Italia kwa mara ya kumi na moja katika muda wa miaka kumi na mbili iliyopita imefuzu kushiriki Kombe la Klabu Bingwa baranai Ulaya.

Milan imeilaza PSV Eindhoven kutoka Uholanzi kwa mabao 3-0.
Baada ya kutoka sare ya 1-1 na Uholanzi katika mechi ya awamu ya kwanza, Kevin Prince alifunga mabao mawili yaliyoiweka timu yake mbele, naye Mario Balotelli akaongezea la tatu na hivyo kuihakikishia mabingwa wa zamani wa kombe hilo nafasi katika raundi ijayo kwa jumla ya mgoli 4-1.
Katika matokeo mengine iliyochezwa siku ya jumatano, Zenit St Petersburg iliikwaruza Pacos Ferreira kwa mabao manne kwa mawili na kufuzu kwa hatua ijayo kwa jumla magoli manane kwa matatu.
Kwingineko, mabingwa wa Jamhuri ya Czech, Viktoria Plzen walishinda wenyeji wao Slovenia Maribor kwa bao moja kwa bila na kujikatia tikiti ya raundi ijayo ya makundi ya kinyang'anyiro cha kuwania Kombe la Klabu Bingwa Barani Ulaya.
Viktoria Plzen imesonga mbele na jumla la magoli 4-1.
Klabu hizo zitajiunga na Arsenal Schalke, Steaua Bucharest na Austria Vienna ambazo zote zilishinda mechi zao siku ya Jumanne katika hatua ya makundi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa