Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ABEL DHAIRA AKALIA KUTI KAVU SIMBA, REKODI YAKE YA KUFUNGWA HII HAPA

KIPA Mganda wa Simba SC, Abbel Dhaira (Pichani) amekwishafungwa mabao 18 katika mechi 11 alizoidakia klabu hiyo tangu Januari mwaka huu alipojiunga nayo, akitokea IBV ya Ligi Kuu ya Iceland, huo ukiwa ni wastani wa karibu mabao mawili kila mechi.


Na mabao mengi aliyofungwa Dhaira yanatokana na mipira ya chini, lakini imeonekana wazi kutokana na urefu wake ni vigumu kumfunga kwa mipira ya juu kipa huyo.

Jumamosi kwenye Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora, Dhaira alifungwa mara mbili kwa mipira ya chini, yote ikiwa mipira ya adhabu wakati Simba SC ikitoka sare ya 2-2 na Rhino Rangers katika mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Hata kocha Mkuu wa Simba SC, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ alisikitishwa na kipa huyo Mganda akisema Abbel Dhaira amewaangusha kwa kufungwa mabao rahisi.

Mechi ya kwanza Dhaira kuidakia Simba SC ilikuwa ni dhidi ya Bandari Uwanja wa Amaan, Zanzibar katika Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu, ambako alifungwa bao moja, timu hiyo ikitoa sare ya 1-1.

Baada ya hapo, akaidakia Simba ikicheza dhidi ya U23 ya Oman, ambako alifungwa moja, timu hiyo ikifungwa 2-1 na akadaka dhidi ya timu ya Jeshi Oman na kufungwa mara mbili, timu hiyo ikilala 3-2. Bao lingine alifungwa Juma Kaseja, ambaye ametemwa msimu huu.

Akadaka tena katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Recreativo de Libolo ya Angola na kufungwa mabao manne, timu hiyo ikilala 4-0.

Akarudi Dar es Salaam na kudaka katika mchezo wa Ligi Kuu msimu uliopita dhidi ya Coastal Union ya Tanga na kufungwa bao moja, timu hiyo ikishinda 2-1.

Akadaka tena katika Ligi Kuu dhidi ya Azam na kufungwa kafungwa mabao mawili, moja la penalti timu hizo zikitoka 2-1, huo ukiwa mchezo wake wa mwisho Simba SC msimu uliopita.

Akarejea kwenye mechi za kujiandaa na msimu huu, akadaka dhidi ya Kahama United mkoani Shinyanga na kwa mara ya kwanza tangu ajiunge na timu hiyo alifanikiwa kumaliza mechi bila kufungwa. Na huo ndio mchezo pekee ambao Dhaira alidaka bila kufungwa Simba SC.

Akadaka tena dhidi ya URA ya kwao, Uganda katika mchezo wa kirafiki na kutunguliwa mara mbili timu hiyo ikilala 2-1 katika mchezo huo wa kirafiki, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Akaenda Tenga kwenye mchezo wa kirafiki na Coastal, akafungwa moja, Wekundu wa Msimbazi wakilala 1-0.

Akadaka tena dhidi ya SC Villa ya kwao, Uganda na kufungwa bao moja, timu hiyo ikishinda 4-1 kabla ya Jumamosi kufungwa mawili katika sare ya 2-2 na Rhino.

Kwa kuwa kipa huyo ndiye chaguo la kwanza la Simba SC kwa sasa, bila shaka na kesho atasimama tena langoni katika mchezo dhidi ya JKT Oljoro mjini Arusha, kwani kipa wa pili Andrew Ntalla aliyesajiliwa kutoka Kagera Sugar msimu huu, bado hajaaminiwa sana.
 
Hakuna shaka Dhaira ni kipa mzuri, lakini inaonekana wazi tangu ametua Simba SC kidogo kiwango chake kimeshuka- pamoja na ukweli kwamba Wekundu wa Msimbazi bado hawajapata safu imara ya ulinzi.

Kisoka, Dhaira aliibukia Express mwaka 2006 ambako alicheza hadi 2008 akahamia URA, alikocheza hadi 2010 akahamia AS Vita ya DRC ambayo ilimuuza IBV mwaka 2012 alikodaka mechi 30 bila kufungwa bao hata moja, hadi anahamia Simba mwaka huu.

Amekuwa akiidakia timu ya taifa ya Uganda tangu mwaka 2009 na tangu 2011 amekuwa kipa namba moja wa timu hiyo, ingawa kwa sasa anakabiliwa na ushindani wa aliyekuwa kipa wa kwanza wa timu hiyo kabla yake, Dennis Onyango pamoja Muwonge Hassan anayeibukia vizuri.

Dhaira alidaka mechi moja tu na kuumia katika Kombe la Challenge mwaka jana na baada ya hapo, Muwonge akadaka hadi kuipa timu ubingwa.

Muwonge tena akaipa Uganda tiketi ya CHAN- na sasa anajitengenezea mazingira mazuri The Cranes mbele ya Onyango na Dhaira.

REKODI YA DHAIRA SIMBA SC:
Simba SC 1-1 Bandari (Kombe la Mapinduzi, alifungwa moja)
Simba SC 0-1 U23 Oman (Kirafiki, alifungwa moja)
Simba SC 1-3 Qaboos (Kirafiki, alidaka nusu akafungwa mawili)
Simba SC 0-4 R. de Libolo (Ligi ya Mabingwa, alifungwa manne)
Simba SC 2-1 Coastal Union (Ligi Kuu, alifungwa moja)
Simba SC 2-2 Azam FC (Ligi Kuu, alifungwa mbili)
Simba SC 1-0 Kahama United (Kirafiki, Kahama hakufungwa)
Simba SC 1-2 URA (Kirafiki, Taifa, alifungwa mbili)
Simba SC 0-1 Coastal (Kirafiki, Tanga alifungwa moja)
Simba SC 4-1 SC Villa (Simba Day, Taifa alifungwa moja)
Simba 2-2 Rhino (Ligi Kuu, alifungwa mbili)

Chanzo cha habari: Bin Zubeiry

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...