Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA USO KWA USO NA MTIBWA UWANJA WA TAIFA, J,TANO

MABINGWA wa Ligi Kuu Vodacom Yanga (Pichani) wanatarajiwa kushuka dimbani Jumatano hii kumenyana na Mtibwa Sugar katika mechi ya kirafiki utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.


Kwa upande wa Yanga, itakuwa ni mechi ya pili ya kirafiki tangu warejee kutoka ziara yao Kanda ya Ziwa ambapo katika mechi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, walitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya URA ya Uganda.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga, zinasema mechi hiyo inayotumika kuijenga zaidi timu hiyo, itachezwa kuanzia 10:00 huku wanachama na wapenzi wa timu hiyo wakijionea ubora wa kikosi chao kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu.

“Yanga kwa sasa kumekuwa na usiri mkubwa hata katika mambo ya msingi, na hiyo inatokana na uongozi ulioko madarakani, lakini mimi nakwambia Jumatano tunacheza taifa kwani najua hivyo,” kilisema chanzo hicho.

Mtandao huu ulifanya mpango kumtafuta Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Baraka Kaziguto, ambaye alisema kuwa yawezekana ikawepo japo hawezi kuthibitisha na alipotafutwa Katibu Mkuu, Laurance Mwalusako, alisema atalizungumzia hilo leo.

Naye Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, alisema yeye taarifa hizo anazo na amejipanga kwa mechi hiyo na kuongeza kuwa hana shaka dhidi ya Yanga kwani ni timu ya kawaida kama nyinginezo.

“Mimi nautambua huo mchezo tunacheza Jumatano na kama ikishindikana tutacheza Jumamosi ila mchezo hupo na mimi nimejipanga ipasavyo,” alisema Mexime.

Aidha, Mexime aliwashangaa viongozi ambao wanalalamikia ratiba ya Ligi Kuu, na kusema kuwa, hata kama mtu ukilalamika kupangwa na timu fulani lazima utacheza nayo tu na kuwataka kuacha imani hizo kwani kila timu lazima icheze.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC