Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WALIOTEMWA SIMBA WAIBUKIA MTIBWA SUGAR

Mshambuliaji aliyeshindwa kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Simba msimu uliopita Abdallah Juma (Pichani), amejiunga na timu ya Mtibwa Sugar inayoshiriki ligi kuu ya Bara ijayo pamoja na beki Paul Ngalema ambaye wamejiunga naye wote kwenye timu hiyo.

Nyota hao waliachwa na Simba baada ya kumalizika kwa msimu wa ligi kuu uliopita kwa madai ya kushuka kwa uwezo wao lakini sasa wataichezea Mtibwa kuanzia msimu ujao.

Akizungumza jana, kocha wa Mtibwa Sugar, Meck Mexime alisema wamewasajili wachezaji hao ili kuziba mapengo ya baadhi ya nyota wake walioiacha timu hiyo na kwenda kujiunga na klabu za Simba na Yanga.

Mbali na Juma na Ngalema ambao wamesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia timu hiyo, Mtibwa imesajili aliyekuwa golikipa namba mbili wa mabingwa wa Bara Yanga, Said Mohamed.

Wachezaji hao kwa pamoja hivi sasa wapo na kikosi cha timu hiyo kilichopiga kambi jijini Dar es Salaam kwa maandalizi ya michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Agosti 24.

Mexime alisema wamemsajili Ngalema ili kuziba pengo la Issa Rashid aliyejiunga na Simba na Juma ambaye Mtibwa ilimuuza kwa Simba mwaka jana, amesajiliwa kuziba nafasi ya Hussen Javu ambaye wiki hii amekamilisha kujiunga na Yanga.

"Said Mohamed yeye tumemsajili ili kuimarisha safu yetu ya ulinzi ili asaidiane na magolikipa waliopo sasa," alisema Maxime.

Aidha, alisema kuwa wanaamini usajili huo utainua viwango vya wachezaji hao amabao wameonekana hawafai walikotoka.

"Tunaamini katika usajili huu, msimu ujao timu zilizowaacha zitakuja tena na kutaka kuwasajili kwa sababu uwezo wao utakua na wataonekana tena bora," alisema Maxime ambaye ni nahodha wa zamani na wa muda mrefu wa Mtibwa na timu ya taifa, Taifa Stars.

Wakati huo huo Mtibwa Sugar itapambana na Yanga  katika mchezo wa kirafiki utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumatano.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC