Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TP MAZEMBE KUMRUDISHA MBWANA SAMATTA SIMBA AGOSTI 8

SIMBA SC jana imeingia kambini Bamba Beach Hotel, Kigamboni, Dar es Salaam kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, inayotarajiwa kuanza Agosti 24, mwaka huu.


Simba SC inayofundishwa na mchezaji wake wa zamani, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ itakuwa huko ikijifua vikali hadi itakapokuja mjini Agosti 8, kwa ajili ya kucheza mechi maalum katika Simba Day.

Bado haijajulikana Simba SC itacheza na nani Agosti 8, lakini habari za ndani zinasema Wekundu hao wa Msimbazi wanaweza kucheza na mabingwa mara nne Afrika, TP Mazembe ya DRC.

Maana yake- kama mechi hiyo itapatikana, mshambuliaji Mbwana Samatta (Pichani) wa Mazembe atacheza dhidi ya timu yake ya zamani kwa mara ya kwanza tangu ahamie DRC mwaka juzi.
   
Simba SC inaingia kambini baada ya Jumamosi kuchapwa mabao 2-1 na URA ya Uganda katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo, uliochezeshwa na refa Michael Magori aliyesaidiwa na Iddi Likongoti na Omar Mfaume wa Dar es Salaam, hadi mapumziko Simba SC walikuwa mbele kwa bao 1-0.

Bao hilo lilifungwa na mshambuliaji mpya, Betram Mombeki aliyegongeana pasi vizuri na Marcel Boniventura. Mombeki alichukua pasi ya Singano ‘Messi’ akawapangua mabeki wa URA kabla ya kumpelekea pasi fupi Marcel aliyemrudishia mshambuliaji huyo mpya, akaunganisha nyavuni.

Baada ya kufunga bao hilo, Mombeki alikwenda kushangilia kwa staili ya mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Nigeria, marehemu Rashid Yakini kwa kuingia kucheza ndani ya nyavu

Kwa ujumla Simba SC ndio waliotawala mchezo kipindi cha kwanza wakionana vema na kucheza kwa kujiamini, wakati kwa URA iliwawia vigumu kuupenya ukuta wa Wekundu wa Msimbazi, uliokuwa chini ya Mganda mwenzao, Samuel Ssenkoom, ambaye ametemwa baada ya mechi hiyo.

Kipindi cha pili, Simba SC inayofundiahwa na kocha mzalendo, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ ilirudi vizuri na kuendelea kuwapa raha mashabiki wake kwa soka maridadi.

Hata hivyo, kibao kiliigeukia Simba SC baada ya mshambuliaji wake, Mombeki kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumpiga kiwiko beki wa URA, Jonathan Mugabi dakika ya 51, ambaye alishindwa kuendelea na mchezo.

Baada ya hapo kwa kuwa tayari mshambuliaji mwingine aliyekuwa akiisumbua ngome ya URA, Zahor Pazi alikuwa amekwishatolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Twaha Ibrahim, mabeki wa timu ya Uganda, wakiongozwa na Joseph Owino anayesajiliwa Simba SC baada ya mechi hiyo na Derick Walullya walianza kupanda zaidi kusaidia mashambulizi.

URA ilipata bao lake la kusawazisha dakika ya 60 mfungaji Lutimba Yayo akiunganisha krosi nzuri ya Walullya.

Wakati SImba wakijaribu kusaka bao la pili, Yayo tena akaifungia URA bao la ushindi dakika ya 75.
 
Hakukuwa tena na mashambulizi ya uhai kwa upande wa Simba na URA hawakuweza kumfunga Mganda mwenzao, Abbel Dhaira zaidi ya mara mbili.

Siku hiyo, kikosi cha Simba SC kilikuwa; Abbel Dhaira, Nassor Masoud ‘Chollo’, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Rahim Juma/Sino Augustino, Samuel Ssenkoom, Jonas Mkude, Ramadhani Singano/Miraj Adam, William Lucian, Betram Mombeki, Zahor Pazi/Twaha Ibrahim na Marcel Boniventura.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...