Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STARS YAAPA KUIGALAGAZA UGANDA KESHO

Nahodha wa timu ya soka ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) (Pichani), Juma Kaseja, amesema wamejiandaa kubadili matokeo kwa kushinda dhidi ya wenyeji Uganda (The Cranes) katika mechi ya marudiano ya kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN) na hivyo kutibua rekodi ya wenyeji ya kutowahi kufungwa nyumbani katika mechi yoyote ya michuano tangu mwaka 2005.


Stars walitua salama nchini Uganda juzi na kuanza maandalizi yao ya mwisho kabla ya kuteremka dimbani kesho kuwakabili wenyeji kwenye Uwanja wa Mandela uliopo jijini Kampala kuanzia saa 10:00 jioni.

Stars iliyolala kwa goli 1-0 katika mechi yao ya kwanza iliyochezwa Julai 13 jijini Dar es Salaam, ina kibarua kizito kesho kwani itatakiwa kushinda walau 2-0 ili kusonga mbele.

Hata hivyo, Kaseja na wenzake wanaamini kuwa wanao uwezo wa kushinda kesho na kuvunja rekodi nzuri ya Cranes kutofungwa kwenye ardhi yao ya nyumbani tangu mwaka 2005. 

Akizungumza na mtandao huu kutokea jijini Kampala jana, Kaseja alisema wachezaji wote kikosini wako ‘fiti’ na wamepania kucheza kufa au kupona kwa nia ya kuibuka na ushindi, hasa baada ya kuwafahamu vyema wapinzani wao kulinganisha na vile ilivyokuwa katika mechi ya kwanza wiki mbili zilizopita.

Kaseja alisema pia wapinzani wao watacheza wakiwa na hofu ya kuwatuliza mashabiki wao ambao wana kiu ya kuona kikosi hicho kinafuzu kushiriki fainali hizo kwa mara ya kwanza.

"Tuko vizuri na tutaweza kubadili ubao wa matokeo. Ni zamu yetu sasa kushinda ugenini kama wao walivyotufunga nyumbani kwetu," alisema Kaseja, akiongeza kuwa salamu za kheri walizopata kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, zimewaongezea morali ya kuibuka na ushindi.

KOCHA POULSEN

Katika hatua nyingine, kocha wa Stars, Kim Poulsen alisema ingawa mechi hiyo ni ngumu, lakini kikosi chake kimejiandaa kuikabili Uganda kwani wachezaji wako wako vizuri na ari kwa ajili ya mechi.

Alisema wachezaji wote wako katika hali nzuri, isipokuwa Khamis Mcha aliyekuwa na maumivu ya goti, lakini kwa mujibu wa madaktari wa timu anaendelea vizuri kwani tayari wanampa mazoezi mepesi.

Kikosi cha kamili cha Stars kilichotua Kampala jana kinaundwa na makipa Juma Kaseja, Mwadini Ali na Ali Mustafa. Mabeki ni Aggrey Morris, David Luhende, Erasto Nyoni, Kelvin Yondani, Nadir Haroub na Vincent Barnabas. Viungo ni Amri Kiemba, Athuman Idd, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Khamis Mcha, Mudhathir Yahya, Salum Abubakar na Simon Msuva. Washambuliaji ni John Boko, Juma Luizio na Mrisho Ngasa.

Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumatatu (Julai 29 mwaka huu). Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC