Ruka hadi kwenye maudhui makuu

STARS TAYARI KUVAANA NA UGANDA, KAPOMBE AITUMIA SALAMU

SAA chache kabla haijashuka dimbani, Uwanja wa Mandela, Namboole mjini hapa, kumenyana na wenyeji Uganda, timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars (Pichani) imetumiwa salamu za heri na beki wake, Shomary Kapombe aliye Uholanzi kwenye majaribio.

Kapombe ametuma salamu hizo kupitia ukurasa wake wa Faceboo, akisema; “Go Taifa Stars, go Bocco, go Ngassa, go Chanongo, go Msuva, go Kiemba...,”.
Ujumbe huu pamoja na kuitakia heri Stars katika mchezo wa jioni hii kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee, pia unawahamasisha baadhi ya wachezaji aliowataja.
Kapombe anawataka John Bocco ‘Adebayor’, Mrisho Ngassa, Haroun Chanongo, Simon Msuva na Amri Kiemba na wenzao wajitume kubeba jahazi la Stars ifuzu CHAN mwakani Afrika Kusini.
Kapombe alikuwepo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wiki mbili zilizopita wakati Stars inafungwa 1-0 na Uganda katika mchezo wa kwanza na baada ya hapo, akaenda Uholanzi kwenye majaribio.
Mchezaji mwingine anayekosekana leo, aliyecheza mechi ya kwanza ni Mwinyi Kazimoto aliyetorokea Qatar.
Kikosi cha Stars kinachotarajiwa kuanza jioni hii ni; Juma Kaseja, Erasto Nyoni, David Luhende, Aggrey Morris, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, John Bocco ‘Adebayor’, Amri Kiemba na Mrisho Ngassa.
Katika benchi watakuwepo Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Luizio, Mudathir Yahya, Nadir Cannavaro, Haroun Chanongo, Simon Msuva na Vincent Barnabas.
Tayari Stars imekwishaingia Uwanja wa Mandela, kiasi cha saa moja iliyopita na muda si mrefu itaingia uwanjani kuamsha misuli. Mungu ibariki Stars, ibariki Tanzania. Amin.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...