Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YATANGAZA MAUZO YA MWINYI KAZIMOTO

Klabu ya soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam imesema kuwa thamani ya kiungo wake nyota, Mwinyi Kazimoto (Pichani), ambaye hivi karibuni alidaiwa kutoroka na kwenda Qatar kufanya majaribio katika klabu ya Lekwhiya inayoshiriki ligi kuu ya nchi hiyo ni dola za Marekani 100,000 (Sh. milioni 160).


Kauli hiyo ya Simba imekuja kufuatia madai kwamba uongozi wa Lekhwiya umeridhishwa na kiwango cha nyota huyo na kuonyesha dalili za kutaka kumsajili.

Kazimoto ambaye tayari amesharejea nchini lakini hajajiunga na kikosi cha Simba kinachojiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, anadaiwa alitoroka nchini akiwa kwenye kambi ya timu ya taifa (Taifa Stars) muda mfupi kabla ya kuelekea Mwanza kuweka kambi ya kujiandaa kwa mechi yao ya wiki iliyopita waliyochapwa ugenini 3-1 dhidi ya Uganda (The Cranes) katika kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani.

Mmoja wa viongozi wa juu wa Simba alisema kuwa baada ya kuelezwa kwa 'mdomo' kwamba klabu hiyo haiko tayari kumsajili Kazimoto kwa dau kubwa, waliwasiliana na kiungo huyo na ndipo alipoamrishwa kurejea nchini.

"Ila walikubali kumlipa mshahara wa dola za Marekani 3,000 (Sh. milioni 4.8), jambo ambalo si baya kama mwenyewe aliridhia... lakini kwa hadhi yake hicho ni kiasi kidogo sana. Wakati tunamsajili kutoka JKT Ruvu tulitumia zaidi ya Sh. milioni 35, lakini sasa thamani yake imepanda," alieleza kiongozi huyo.

Akizungumza jana, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kwamba hajapokea barua rasmi kutoka timu yoyote ndani au nje ya nchi ikieleza nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.

Mtawala alisema kwamba mbali na kuharibu programu za kikosi cha Stars, pia kutokuwapo kwa Kazimoto kambini kutamvuruga kocha Abdallah Kibaden 'King' ambaye alipaswa kuwa na kikosi kamili wakati huu ili kujiandaa na Ligi Kuu ya Bara.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC