Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YAINGIZWA MKENGE, YATOSA NYOTA WAKE WOTE WA KIGENI

Mussa Mudde kulia akiwa na aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Simba Nyange Kaburu
Uongozi wa klabu ya Simba umewatosa jumla wachezaji wote wa kigeni waliokuwa wakijaribiwa kwa matumaini ya kuwamo katika kikosi chao cha Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu ujao (2013/2014) huku pia ikisitisha mkataba wa Mganda Musa Mude aliyeichezea timu yao msimu uliopita, imeelezwa jana.


Mude aliingia mkataba wa miaka miwili na Simba mwaka jana na hivyo kabla ya kusitishiwa mkataba wake, alibakiza mwaka mwingine mmoja kuichezea klabu hiyo ya 'Wekundu wa Msimbazi'.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema tayari mchezaji huyo ameshalipwa haki zake zote na pia kukabidhiwa tiketi ya ndege ya kurejea nyumbani kwao Uganda juzi.

Mude ambaye alikuwamo katika kikosi cha Simba kilichomaliza katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa mwisho wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu uliopita, hakupatikana jana kuzungumzia kuachwa kwake na pia hatma yake baada ya kuondoka Msimbazi.

Katika hatua nyingine, Mtawala alisema vilevile kuwa klabu hiyo imeachana na mpango wowote wa kutaka kuwasajili wachezaji wengine wa kigeni waliokuwa wakiwafanyia majaribio ambao ni pamoja na Waganda Samuel Ssenkoomi na Assumani Buyinza, Felix Cuipo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na James Kun kutoka Sudan Kusini.

Katibu huyo aliongeza kuwa maamuzi ya kuwaacha Mudde na kina Ssenkoomi yamefanywa na kamati yao ya usajili iliyo chini ya mwenyekiti wake, Zacharia Hanspoppe; ikiwa ni baada ya kupokea maelekezo kutoka kwa benchi la ufundi kwamba wachezaji hao hawajaonyesha viwango vya juu kwa namna ilivyotarajiwa.

Kutokana na maamuzi hayo mazito ya uongozi wa Simba, sasa kikosi chao kimebakiwa na wageni wawili tu ambao ni kipa wa kimataifa wa Uganda, Abel Dhaira na Mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya Burundi msimu uliopita, Mrundi Amissi Tambwe aliyesajiliwa kutoka Vital'O ya Burundi.

Habari zaidi kutoka ndani ya klabu hiyo zinaeleza kwamba uongozi wa klabu hiyo umeanza mazungumzo na beki wa Uganda, Joseph Owino ambaye aliwahi kuichezea Simba na sasa akiitumikia klabu ya URA inayoshiriki Ligi Kuu ya Uganda.

Owino ambaye pia aliwahi kuichezea klabu ya Azam anadaiwa kutaja dau kubwa na sasa viongozi wa 'Wanamsimbazi' wanaendelea kuzungumza naye ili wafikie makubaliano na mwishowe kumsajili baada ya kuvutiwa na kiwango cha juu alichoonyesha wakati URA ilipocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Taifa wiki iliuopita na kuwaadhiri wenyeji kwa kuwachapa 2-1.

Pia klabu hiyo inadaiwa iko katika mazungumzo kwa nia ya kumsajili Mganda Moses Oloya anayecheza soka la kulipwa nchini Vietnam ili ajiunge na Simba katika kipindi cha usajili wa dirisha la Novemba, 2013.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC